Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza na kukamilisha ujenzi wa mradi wa maji toka Ziwa Victoria kwenda Biharamulo?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwanza kabisa nimshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri, na especially commitment ya Serikali kwamba Mradi huu wa Maji ya Ziwa Victoria unaanza katika mwaka wa fedha huu wa 2023/2024. Lakini kama ulivyosema, utekelezaji wa miradi ya maji kwa Biharamulo uko asilimia 65 sasa hivi.

Mheshimiwa Spika, sasa ninaomba, umesema mmetuwekea 2.8 kilometa mtandao. Sasa kwa sababu maji yanakuja, naomba ufanye commitment, kwa sababu sasa bahati nzuri leo najibiwa na Waziri mwenyewe, angalau uniongezee kilometa tatu nyingine waweze kusambaza mabomba zaidi pale mjini ili maji yatakapofika yawafikie wananchi wengi zaidi. Swali la kwanza hilo, naomba tu commitment.

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Mradi huu wa Maji wa Ziwa Victoria tulikuwa tumeahidiwa pia kutoa maji Ziwa Victoria tupite katika Kata za Nyamigogo, yale Kabindi, Nyabusozi, Nemba yaende Nyantakara yafike mpaka Nyakanazi katika kata ya Lusahunga. Sasa ni lini mradi huu wa kutoa maji za Ziwa Victoria katika line hii ya kuyapeleka mpaka Nyakanazi utatekelezwa na Serikali kwa ajili ya wakazi wa Buharamulo na hususan Nyakanazi, center kubwa inayokuwa pale?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge na kipenzi cha Wanabiharamulo, kwa kazi kubwa ambayo anaifanya. Nimhakikishie kwamba Wizara ya Maji jukumu letu ni kuhakikisha Wanabiharamulo wanapata maji. Kwa hiyo, juu ya ombi lake la kuongeza mtandao, tupo tayari kutoa fedha kwa ajili ya uongezaji wa mtandao wananchi wake waweze kupata huduma ya maji safi na salama.

Mheshimiwa Spika, swali la pili; ni juu ya ujenzi huu wa mradi mkubwa. Ujenzi wa mradi huu chanzo tunachukua pale eneo la Chato na ni miongoni mwa miradi ya miji 28 na mkandarasi amekwishapatikana, advance payment imekwisha tolewa. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba safari moja huanzisha mwingine, uanzaji wa mradi huu ndiyo tunakwenda kukamilisha ujenzi wa mradi wa Biharamulo, ahsante sana.