Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 19 Water and Irrigation Wizara ya Maji 240 2023-05-05

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: -
Je, lini Serikali itaanza na kukamilisha ujenzi wa mradi wa maji toka Ziwa Victoria kwenda Biharamulo?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Engineer Ezra John Chiwelesa, Mbunge wa Jimbo la Biharamulo Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hali ya upatikanaji wa huduma ya maji kwa Mji wa Biharamulo ni asilimia 86. Katika kupunguza kero ya maji kwa wakazi wa mji huo, Serikali ina mipango ya muda mfupi na mrefu. Katika mpango wa muda mfupi, Serikali inaendelea kutekeleza mradi wa kuboresha miundombinu ya maji Biharamulo, na kazi zinazotekelezwa ni pamoja na ujenzi wa chujio, bomba kuu la urefu wa kilomita 2.8, tanki la ujazo wa lita milioni moja na ununuzi wa pampu yenye uwezo wa kusukuma maji lita laki 120 kwa saa. Utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 65 na unatarajia kukamilika mwezi Juni, 2023 na kuongeza huduma ya maji kufikia asilimia 90.

Mheshimiwa Spika, katika mpango wa muda mrefu, Serikali itajenga mradi mkubwa wa kutoa maji Ziwa Victoria kwenda Biharamulo. Usanifu wa mradi huo umekamilika na ujenzi unatarajiwa kuanza katika mwaka wa fedha 2023/24.