Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ng'wasi Damas Kamani

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NG’WASI D. KAMANI aliuliza: - Je, Serikali haioni umuhimu wa kutoa kipaumbele cha ajira kwa vijana wanaojitolea kutumikia katika kada mbalimbali za utumishi?

Supplementary Question 1

MHE. NG'WASI D. KAMANI: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, moja, kwa vile wakati tunapitisha bajeti ya Wizara hii, Wabunge wengi ambao ni wawakilishi wa wananchi walionesha haja ya kuiomba Serikali kuwaangalia vijana mbalimbali wanaojitolea kwa jicho la tatu, hasa katika maombi ya kazi, na kwa vile Serikali yenyewe ndiyo imesema kwamba ilitengeneza mazingira haya ili kuwapa competitive advantage vijana hawa wanapotoa nafasi za kazi, swali la kwanza: -

Je, Serikali haioni haja ya kuja na mabadiliko ya hizi sera, kanuni au sheria ili kuweka hii competitive advantage kwa hawa vijana pindi maombi ya kazi yanapopelekwa?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, nini sasa kauli au commitment ya Serikali kwa vijana mbalimbali waliopo katika vituo mbalimbali vya kazi sasa wakiwa wanajitolea kutoa huduma mbalimbali kwa Watanzania?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA
UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ng'wasi Damas Kamani, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza kabla sijajibu maswali yake ya nyongeza, nataka nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa jinsi ambavyo hajawasahau vijana wake, na kwa kweli anafanya kazi nzuri, na Mwenyezi Mungu atakujalia dada yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, maelezo ya ziada aliyoyatoa Mheshimiwa Ng’wasi Kamani ninaunaga naye moja kwa moja, ni kweli Bunge lako wakati linajadili Hotuba ya Bajeti hii ya Wizara yetu ya Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Wabunge wengi walizungumza sana juu ya jambo la vijana wanaojitolea. Na nataka nirudie tena kueleza kwa kifupi juu ya commitment ya Serikali.

Mheshimiwa Spika, Serikali ilikiri kupokea maoni ya Wabunge wote na kwamba tutakwenda kuyafanyia kazi. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ninapozungumza leo saa nane kikao cha kwanza kwa ajili ya kujadili jinsi gani Serikali inakabiliana na tatizo la ajira tunakwenda kuanza chini ya uongozi wangu, kwa sababu Mheshimiwa Waziri amenikasimia mamlaka hayo niweze kulisukuma mbele jambo hili la ajira kwa vijana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pili, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwenye swali lake la pili juu ya commitment ya Serikali; kwa maelezo niliyotangulia kutoa hapa, ni wazi kwamba Serikali inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, imejizatiti kuhakikisha kwamba inakabiliana na jambo hili, na tuko bega kwa bega naye Mheshimiwa Rais sisi kama watendaji wake, kuhakikisha kwamba tunakwenda kuli-address jambo hili na kulitafutia mwarobaini wake.

Name

Janejelly Ntate James

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NG’WASI D. KAMANI aliuliza: - Je, Serikali haioni umuhimu wa kutoa kipaumbele cha ajira kwa vijana wanaojitolea kutumikia katika kada mbalimbali za utumishi?

Supplementary Question 2

MHE. JANEJELLY J. NTATE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri kwa niaba ya Serikali; je, sasa kwenye Ajira Portal ni lini mtaongeza key ambayo itam-pick yule kijana ambaye amejitolea ikawa ni sifa ya nyongeza katika kuajiriwa? (Makofi)

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA
UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Janejelly James Ntate, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba kurejea tena kwenye maelezo yaliyotolewa na Mheshimiwa Waziri wakati anafunga mjadala wa hoja ya Wizara yetu wakati wa bajeti. Alieleza na ninaomba ni- quote kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri alieleza kuwa; Serikali imeyachukua maoni yote yaliyotolewa na Wabunge, na kwamba tunakwenda kuyafanyia kazi na utakapofika muda wa kuwashirikisha Wabunge kama wadau kwa kutoa maoni juu ya mfumo mzuri wa kutoa ajira kwa vijana wetu ambao mawazo mazuri kama haya anayoyatoa Mheshimiwa Mbunge yataingizwa ndani yake, tutakuja kulishirikisha Bunge lako na Wabunge watapata nafasi hiyo ya kueleza yale yote ambayo wanayataka yaingie katika mfumo.