Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 19 Public Service Management Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 239 2023-05-05

Name

Ng'wasi Damas Kamani

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NG’WASI D. KAMANI aliuliza: -

Je, Serikali haioni umuhimu wa kutoa kipaumbele cha ajira kwa vijana wanaojitolea kutumikia katika kada mbalimbali za utumishi?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, naomba kujibu Swali Na. 239, lililoulizwa na Mheshimiwa Ng’wasi Damas Kamani, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali iliweka mazingira ya kuwawezesha vijana wanaohitimu katika vyuo mbalimbali kujitolea katika Taasisi za Umma kwa lengo la kuwawezesha kujipatia sifa za ziada zitakazowawezesha katika ushindani pindi nafasi mbalimbali za ajira zinapotangazwa. Hata hivyo, kwa mujibu wa Kifungu Na. 2.1.2 cha Sera ya Menejimenti ya Ajira katika Utumishi wa Umma, Toleo la Pili la Mwaka 2008 na Kanuni D. 6 ya Kanuni za Kudumu za Utumishi wa Umma za Mwaka 2009 ikisomwa pamoja na Kanuni Namba 12(1) ya Kanuni za Utumishi wa Umma za Mwaka 2022, ajira kwa nafasi zilizo wazi katika Utumishi wa Umma hujazwa kwa ushindani na uwazi kwa kufanya usaili na kupata washindi katika nafasi husika.

Mheshimiwa Spika, hivyo, nitumie nafasi hii kuwashauri na kuwahamasisha vijana wanaojitolea katika kada mbalimbali za utumishi wenye sifa stahiki, kuomba nafasi za kazi pindi zitakapotangazwa ili waweze kushindana na waombaji wengine wenye sifa stahiki.