Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kupeleka maji ya Ziwa Victoria katika Kata za Ikunda, Mwakata, Menga, Shilela na Lunguya - Msalala?

Supplementary Question 1

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi hii ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Waziri mradi wa Nduku - Msangi – Ntobo ni mradi ambao umechukua muda mrefu sana, kwa hatua iliyofikiwa sasa wameweza kukosa kiasi cha Shilingi Milioni 50 tu kwa ajili ya Mkandarasi kuchimba mtaro, kuchelewa kwa mradi huu kumesababisha sasa Hospitalli ya Wilaya ya Ntobo kukosa maji na hivyo kupelekea mlipuko wa magonjwa mbalimbali kwenye hospitali ile ya Wilaya.

Je, ni lini sasa Wizara itatoa kiasi hiki kwa dharura ili ipeleke fedha hizo hospitali ya Wilaya iweze kupatiwa maji?

Swali langu la pili, Kata niliyoitaja hapa kwa maana ya Mwakata imepitiwa na bomba kuu linalotoka Kagongo kwenda Isaka na Kata hii haina maji. Je, ni nini sasa mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba Kata hii na yenyewe inanufaika na maji hayo kwa sababu bomba hilo limepita maeneo hayo? Ahsante.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge Kaka yangu wa Msalala kwamba Wizara ya Maji mwezi huu tumepokea Bilioni 67 kwa ajili ya malipo ya Wakandarasi. Kwa hiyo, moja ya maeneo ambayo tutayapa kipaumbele cha haraka ni eneo la Msalala kuhakikisha mradi huu unakamilika na wananchi wanapata huduma ya maji safi na salama.

Mheshimiwa Naibu Spika, eneo la pili ni juu ya mradi ambapo bomba kuu linapita. Sera inasema bomba kuu linapopita vijiji ambavyo vipo karibu na kilomita 12 kulia na kushoto mwa bomba kuu, vinahakikishiwa kwamba vinapata huduma. Nataka nimhakikishie hili tumelipokea na tunaenda kulifanya kazi kuhakikisha kwamba Kata hiyo nayo inapata huduma ya maji safi na salama.

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kupeleka maji ya Ziwa Victoria katika Kata za Ikunda, Mwakata, Menga, Shilela na Lunguya - Msalala?

Supplementary Question 2

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Mheshimiwa Waziri ulituahidi mwaka jana kwenye Bunge la Bajeti ungetuchimbia visima katika shule za Kata ndani ya Manispaa ya Iringa, ulipokuja kwenye Wizara Rais mwezi wa Agosti uliahidi kuleta gari katika Mkoa wa Iringa ili tuweze kupata huduma hiyo ya visima, sasa hatijachimbiwa visima mpaka leo.

Swali langu ni; kwanza, huogopi kwenda motoni?

Namba Mbili; mnatuchimbia lini visima?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nitumie nafasi hii kumshukuru sana Mheshimiwa Rais, tuliomba kuwa na magari kwa ajili ya uchimbaji visima katika kila Mkoa, magari yale tumekwishayapata na katika kila Mkoa tumekwishayapeleka. Ninamuomba Mheshimiwa Mbunge katika yale maeneo ambayo anaona tunahitaji uchimbaji visima, kwa sababu vitendea kazi tunavyo, hatuna kisingizio chochote. Kwa hiyo, jukumu letu ni kuhakikisha maeneo ambapo panatakiwa kuchimbiwa visima tunakwenda kuchimba visima. Ahsante sana.

Name

Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kupeleka maji ya Ziwa Victoria katika Kata za Ikunda, Mwakata, Menga, Shilela na Lunguya - Msalala?

Supplementary Question 3

MHE. ASK. JOSEPHAT M. GWAJIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na mradi mkubwa wa maji unaotokea Ruvu Chini kukamilika lakini baadhi ya Kata za Jimbo la Kawe kama Mbezi Juu hazina maji kabisa. Nini kauli ya Serikali?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nitumie nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Mbunge, kubwa mradi ule mkubwa tumeshaukamilisha na Mheshimiwa Waziri Mkuu katika wiki ya maji alikuja kuuzindua, kazi iliyobaki ni suala zima tu la usambazaji. Kwa hiyo, kikubwa tutaongeza kasi juu ya usambazaji maeneo haya ya Mbezi Juu na maeneo mengine kuhakikisha kwamba wanapata huduma ya majisafi na salama.

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kupeleka maji ya Ziwa Victoria katika Kata za Ikunda, Mwakata, Menga, Shilela na Lunguya - Msalala?

Supplementary Question 4

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Mkoa wa Tabora ni moja kati ya Mikoa ambayo imenufaika na mradi wa maji ya Ziwa Victoria. Jimbo la Tabora Mjini ni moja kati ya Majimbo hayo ambayo yamepata maji hayo lakini Kata zilizoko pembezoni mpaka sasa hazijanufaika na maji hayo.

Je, Serikali mna mpango gani wa kupeleka fedha ili iwasaidie kusambaza maji na wananchi wetu waweze kunufaika na mradi huo?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ninamshukuru Mheshimiwa Mbunge kwa kuthamini kazi kubwa ambayo imefanywa na Serikali, kulikuwa na mradi mkubwa zaidi ya Bilioni 600 kuyatoa maji Ziwa Victoria kuyapeleka Tabora, Nzega hadi Igunga. Nataka nimhakikishie maeneo hayo yote ya pembezoni ambayo yanahitaji maji tutayafikia kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya majisafi na salama na tutatoa fedha Mheshimiwa Mbunge. (Makofi)