Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 16 Water and Irrigation Wizara ya Maji 211 2023-05-02

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kupeleka maji ya Ziwa Victoria katika Kata za Ikunda, Mwakata, Menga, Shilela na Lunguya - Msalala?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Iddi Kassim Iddi Mbunge wa Msalala, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekamilisha usanifu wa upanuzi wa miradi ya maji ya Mhangu - Ilogi na Nduku - Busangi itakayohudumia Kata za Ikunda, Mwakata, Menga, Shilela na Lunguya zilizopo Wilayani Msalala. Kwa sasa taratibu za kumpata Mkandarasi kwa ajili ya ujenzi zinaendelea na ujenzi utaanza katika mwaka wa fedha 2023/2024.