Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amandus Julius Chinguile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nachingwea

Primary Question

MHE. AMANDUS J. CHINGUILE K.n.y. MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa mradi wa maji wa Kihesa Mgagao, Masege hadi Masalali - Kilolo?

Supplementary Question 1

MHE. AMANDUS J. CHINGUILE: Mheshimiwa naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri nina maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa, kuna baadhi ya vitongoji katika vijiji hivyo havijawekwa kwenye orodha ya mpango wa kuwekewa vitu kwa ajili ya kuchotea maji. Je, Serikali inaweza kupokea maombi mapya sasa maalum kwa ajili ya kuongeza vituo vya kuchotea maji kwenye vijiji ambavyo vimepitiwa na mradi huu?

Swali la pili, miradi mingi kwenye Halmashauri zetu imekwama kwa sababu ya upatikanaji wa mabomba ambayo yananunuliwa kwa pamoja kupitia RUWASA Makao Makuu.

Je, Serikali sasa inatuhakikishiaje kwamba mabomba sasa yanakwenda kupatikana kwa wakati ili kutokukwamisha miradi mingi kwenye Halmashauri zetu?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, moja ya jukumu mahsusi na Wizara ya Maji ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji safi na salama, tunao huu mradi mkubwa ambao unajengwa na kuna baadhi ya vitongoji ameviainisha ambavyo vinahitaji maji, nataka nimhakikishie kukamilika kwa mradi huu na hivyo vitongoji navyo vitapokea kuhakikisha nao wanapata huduma ya maji safi na salama. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Maji kupitia Wakala wa Maji Vijijini ni kuhakikisha tunatatua changamoto ya maji katika maeneo ya vijijini. Tulikuwa na changamoto ya manunuzi na tumepewa ombi na maelekezo ya Bunge ni kuhakikisha manunuzi haya yanafanyika katika maeneo ya Mikoa, tulishakaa na wenzetu wa manunuzi kwa maana ya RUWASA maelekezo ya Wizara ni kwamba manunuzi yote yanatakiwa kufanyika katika Mikoa husika ili kuharakisha utekelezaji wa miradi. (Makofi)

Name

Dr. Florence George Samizi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Primary Question

MHE. AMANDUS J. CHINGUILE K.n.y. MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa mradi wa maji wa Kihesa Mgagao, Masege hadi Masalali - Kilolo?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kunipatia nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mnamo mwaka 2021 Mheshimiwa Waziri Mkuu aliweka Jiwe la Msingi wa ujenzi wa mradi wa maji katika Kijiji cha Kifura ambao wakati huo ulikuwa asilimia 43, mpaka leo mradi huo umetelekezwa na uko asilimia 43 hiyohiyo. Je, ni nini mpango wa Serikali kutenga fedha ili kukwamua mradi huu wa maji ili wananchi wa Kifura waweze kupata maji?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ninampongeza Mheshimiwa Mbunge, kubwa mradi huu wa Kifura ni mradi ambao ulikuwa unatekelezwa na kampuni ya Nangai pamoja na taasisi ambayo inaitwa ENABEL, tulikuwa na changamoto baina ya huyu Mkandarasi na hii taasisi, tumekwisha kaa nao na moja ya maelekezo ambayo tumempatia yule Mkandarasi, Tarehe 31 Agosti, akabidhi mradi huo ili wananchi wa Kifura waendelee kupata huduma ya maji safi na salama.(Makofi)

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. AMANDUS J. CHINGUILE K.n.y. MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa mradi wa maji wa Kihesa Mgagao, Masege hadi Masalali - Kilolo?

Supplementary Question 3

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza nianze kuipongeza Serikali ya Mama Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kusambaza maji vijijini. Je, wizara iko tayari kushusha bei ya maji Wilaya ya Nyang’hwale kutoka 1,700 kwa unit na kufanya iwe 1,500 ili kuhamasisha wananchi wengi kuweza kujiunga na mtandao huo wa maji? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ni haki ya mwananchi kupata huduma ya maji lakini mwananchi naye asisahau anao wajibu wa kulipia bill za maji. Kwa hiyo, ameonesha hiyo changamoto na nimuombe basi Saa Saba tuweze kukaa na timu yetu tuone namna nzuri ya kuhakikisha wana Nyang’hwale tunatatua changamoto hiyo. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. AMANDUS J. CHINGUILE K.n.y. MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa mradi wa maji wa Kihesa Mgagao, Masege hadi Masalali - Kilolo?

Supplementary Question 4

MHE. MIRAJI J. MTATURU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naishukuru sana Serikali kwa kutusaidia kuweka miradi ya maji kwenye vijiji takribani Vinne kikiwemo Kijiji cha Matare pale katika Jimbo la Singida Mashariki. Hoja yangu na swali langu Mheshimiwa Waziri, mradi umekamilika na Mkandarasi amemaliza kazi changamoto iko kwenye umeme na tumeshalipia watu wa TANESCO mpaka leo umeme haujawekwa.

Je, ni lini Serikali itahakikisha umeme unawekwa ili wananchi wa Matare waanze kutumia maji. (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, Wizara ya Maji inafanya kazi kwa ukaribu sana na Wizara ya Nishati na wamekuwa msaada mkubwa kwetu, hili jambo tutalifuatilia kwa haraka kuhakikisha ujenzi wa eneo hilo linakamilika kwa haraka. Ahsante sana.

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMANDUS J. CHINGUILE K.n.y. MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa mradi wa maji wa Kihesa Mgagao, Masege hadi Masalali - Kilolo?

Supplementary Question 5

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kuniona. Mradi wa Maji Kyerwa, Nyaruzumbula mpaka Kamuli ni lini utaanza?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kama nilivyoeleza Tarehe 10 mwezi Mei, tunawasilisha bajeti yetu, nataka nimhakikishie kama Mheshimiwa Rais alivyosema mambo ni moto, mambo ni fire tutakwenda vizuri katika kuhakikisha jambo hili linaenda vizuri. Ahsante sana. (Makofi)