Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 16 Water and Irrigation Wizara ya Maji 210 2023-05-02

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. AMANDUS J. CHINGUILE K.n.y. MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa mradi wa maji wa Kihesa Mgagao, Masege hadi Masalali - Kilolo?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Justin Lazaro Nyamoga, Mbunge wa Kilolo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa mradi wa maji katika vijiji vya Kihesa Mgagao, Masege hadi Masalali upo kwenye hatua za mwisho za kumwajiri Mkandarasi. Utekelezaji wa mradi utaanza Mwezi Mei, 2023 na unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Mei, 2024. Kazi zitakazofanyika ni pamoja na ujenzi wa matenki matatu (3) yenye jumla ya ujazo wa lita 250,000, ujenzi wa mtandao wa mabomba ya maji yenye urefu wa kilometa 25.4 na ujenzi wa vituo 25 vya kuchotea maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, kukamilika kwa mradi huo kutanufaisha wananchi wapatao 9,006 waishio kwenye vijiji hivyo.