Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuvipatia maji Vijiji vilivyopo mwambao wa Ziwa Nyasa?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza ninashukuru sana Serikali kwa jitihada ambazo zimeshaanza kufanyika katika ukanda wa Ziwa Nyasa. Kwa kuwa, Jimbo hili lina pande kuu mbili za Umatengo na Ziwa Nyasa, katika eneo hili la Umatengo kuna Kata ya Lumeme Kijiji cha Luhindo, Uhuru na Mipotopoto lakini pia Kata ya Luhangalasi zina tatizo kubwa sana la maji.

Je, Wizara ina mpango gani wa kupeleka fedha za dharura kwa ajili ya kuvisaidia vijiji hivi angalau hata kama ni Shilingi Milioni Moja.

Swali la pili, katika ukanda wa mwambao uliozungumzia kuna Kijiji cha Mtupale na Chiwimbi hivi havijazungumzwa, Je, mpango wa Serikali ni nini ili kuhakikisha na wenyewe wanapata maji? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa kazi kubwa anayoifanya, Wizara ya Maji pamoja na mpango mkakati wa kuhakikisha tunatumia rasilimali toshelevu, kwa maana ya mito na maziwa Wizara ya Maji imejipanga sasa hivi tuna mitambo katika kila Mkoa, moja ya maelekezo ambayo niyatoe na tunashirikiana na Mheshimiwa Mbunge eneo hilo ambapo kama kuna tuwezekano wa kupata maji ya kisima basi tutachimba kwa haraka kuhakikisha wananchi wake wanaanza kupata huduma ya maji safi na salama.

Mheshimiwa Naibu Spika, kubwa nataka nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge, tarehe 10 Mei, bajeti yetu ya Wizara ya Maji tunawasilisha kwa hiyo moja ya mikakati mizuri ambavyo tumejipanga ni kuhakikisha tunakamilisha changamoto ya maji kwa kiwango kikubwa sana. Ahsante sana.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuvipatia maji Vijiji vilivyopo mwambao wa Ziwa Nyasa?

Supplementary Question 2

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipatia nafasi niulize swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na fedha ya dharura iliyotoka Wizarani kwako Mheshimiwa Waziri, bado haijamaliza changamoto ya maji Jimbo la Nkasi Kaskazini. Tunapenda kufahamu mchakato wa kutoa maji Ziwa Tanganyika kusambaza kwenye Mkoa wa Rukwa umefikia wapi?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nchi yetu Mwenyezi Mungu ameijalia tuna rasilimali za maji juu ya ardhi na chini ya ardhi mita za ujazo bilioni 126, maji yaliyokuwa juu ya ardhi ni zaidi ya mita za ujazo bilioni 105. Maelekezo ya Mheshimiwa Rais ni kuhakikisha tunatumia rasilimali hizi toshelevu kwa ajili ya kutatua matatizo ya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa mpango mkakati wa Wizara yetu ya Maji na tutawasilisha katika bajeti yetu ya Terehe Kumi Mwezi wa Tano ni kuhakikisha tunatumia Ziwa Tanganyika kwa ajili ya kutatua matatizo ya maji Kigoma, Mkoa wa Rukwa na Mkoa wa Katavi. Ahsante sana. (Makofi)