Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 16 Water and Irrigation Wizara ya Maji 209 2023-05-02

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuvipatia maji Vijiji vilivyopo mwambao wa Ziwa Nyasa?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika; naomba kujibu swali la Mheshimiwa Engineer Stella Martin Manyanya, Mbunge wa Ziwa Nyasa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Mwambao wa Ziwa Nyasa una vijiji 39 na kati ya hivyo vijiji 18 vinapata huduma ya maji na vijiji 21 havina. Katika mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali inatekeleza Miradi ya Maji ya Lituhi, Liuli, Ngumbo, Puulu, Songambele na Nangombo-Kilosa, inayotarajia kukamilika katika mwaka wa fedha 2023/2024 na kunufaisha vijiji 17.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile, Serikali ipo katika hatua za mwisho kukamilisha usanifu wa Mradi wa Maji Ndengele-Mbuyula utakaohudumia vijiji vitatu na itaendelea na usanifu katika Kijiji cha Ndonga. Ujenzi wa miradi hii utafanyika katika mwaka wa fedha 2023/2024.