Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Edwin Maleko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika Vijiji na Vitongoji vya Mkoa wa Kilimanjaro ambavyo havina huduma ya umeme?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER E. MALLEKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza.; je, ni vigezo gani vinatumika kupanga ugawaji wa umeme kwa urban peri -urban pamoja na REA?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; ni upi mpango wa Wizara katika kushughulikia malalamiko ya wananchi juu ya tariff kwa bei za umeme kuwa kubwa?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Esther Malleko, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye eneo la kwanza, TANESCO imekuwa ikipanga Mradi wa REA uende wapi na Peri-Urban uende wapi kulingana na taarifa zinazotolewa na TAMISEMI. Pia wenzetu wa TAMISEMI ndio wenye dhamana ya kusema hapa ni mjini na hapa ni kijijini, hapa ni Halmashauri ya Mji, hapa ni Jiji na hapa ni Manispaa. Kwa hiyo, sisi TANESCO tumekuwa tukipata taarifa za TAMISEMI na tunatumia hizo kupeleka Miradi ya Peri-Urban kwenye maeneo ya mijini na Miradi ya REA kwenye maeneo ya vijijini. Pia tumeendelea kushirikiana nao kubaini maeneo jinsi yanavyobadilika ili tuweze kufikisha huduma sahihi kwa wakati.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye swali la pili, katika hizi nchi za jirani na Tanzania, watu wenye bei za chini kabisa za umeme ambazo kimsingi kabisa zimewekewa ruzuku na Serikali ni Tanzania. Gharama za uzalishaji na usambazaji wa umeme Tanzania haziko na usawa na uwiano sahihi na gharama zinazolipwa na wananchi katika kupata ile huduma ya umeme na kuunganishwa. Kwa hiyo, gharama zetu ziko chini na sisi tunadhani kuna haja ya kuzitazama vizuri ili shirika liweze kuendelea kujiendesha na kuweza kutoa huduma sahihi kwa wananchi na kwa wakati.

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika Vijiji na Vitongoji vya Mkoa wa Kilimanjaro ambavyo havina huduma ya umeme?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHRISTINE C. MNZAVA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuwa Serikali iliahidi kuvipatia umeme vijiji vilivyopo katika Kata ya Mwamalili, Kolandoto, Chibe, Mwawaza na Old Shinyanga; je, ni lini Serikali itavipatia umeme vijiji hivyo?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mnzava, Mbunge wa Viti Maalum, Shinyanga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, vijiji vyote ambavyo havikuwa na umeme na havina umeme hadi sasa viko katika Mradi Mkubwa wa Umeme wa REA, awamu ya tatu, mzunguko wa pili. Kufikia Desemba, 2023 tuna uhakika vijiji hivyo vitakuwa vimepata umeme kupitia mikataba ambayo tuko nayo na inayoendelea kutekelezwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mradi huo ndio tunamshukuru Mheshimiwa Rais, Samia Suluhu Hassan kwa kuongeza kilomita mbili katika ile kilomita moja tuliyokuwa nayo awali. Kwa hiyo wigo wa mradi utakuwa ni mpana zaidi kuweza kuwafikia wananchi wengi katika vitongoji kwa ajili ya kupata maendeleo kwenye maeneo yao.

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika Vijiji na Vitongoji vya Mkoa wa Kilimanjaro ambavyo havina huduma ya umeme?

Supplementary Question 3

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Naibu Spika, naishukuru Serikali kwa kuwasha umeme kwa wakati katika vijiji vya Jimbo la Meatu hususani kwenye kata ambazo zilikuwa hazijaguswa. Je, ni lini sasa Serikali itaanza kusambaza umeme wa ujazilizi katika vitongoji vyote vya Jimbo la Meatu?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Leah Komanya, Mbunge wa Meatu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza tunashukuru kwa pongezi angalau kuna maeneo ambapo Mradi wetu wa REA III, round II umekamilika ikiwemo Mkoa wa Simiyu na tunaendelea kuhakikisha kwamba na maeneo mengine mradi unakamilika. Katika vitongoji kama nilivyotangulia kusema tayari tumepata fedha kwa ajili ya kuongeza wigo kutoka kilomita moja hadi kilomita tatu ambazo zitafika katika vitongoji vingi zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, Serikali inatafuta fedha nyingi zaidi za kuweza kupeleka umeme kwenye vitongoji vyote takribani 36,000 ambavyo vimebaki Tanzania visivyokuwa na umeme takribani shilingi 6,500,000,000,000 na tunaamini zitapatikana na umeme katika miaka minne, mitano au sita ijayo, vitongoji vyote Tanzania vitafikiwa na huduma ya umeme.