Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 16 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 207 2023-05-02

Name

Esther Edwin Maleko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika Vijiji na Vitongoji vya Mkoa wa Kilimanjaro ambavyo havina huduma ya umeme?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Esther Edwin Malleko, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimwa Naibu Spika, Mkoa wa Kilimanjaro una jumla ya vijiji 519 ambapo mpaka sasa vijiji 11 tu havina umeme. Vijiji hivi vimepangwa kupatiwa umeme kupitia Mradi wa REA, awamu ya tatu, mzunguko wa pili, ambao unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba, 2023.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Kilimanjaro una vitongoji 2,260 na kati ya hivyo, vitongoji 286 tu ndiyo havina umeme. Vitongoji hivyo vitaendelea kupatiwa umeme kupitia Miradi ya Ujazilizi kwa kadri fedha zitakavyopatikana, ahsante.