Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapa pembejeo wakulima wa mbogamboga nchini?

Supplementary Question 1

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; Masoko ya Wilaya ya Lushoto hupoteza zaidi ya tani 400 za mbogamboga na matunda kwa kila mwezi. Je, Serikali haioni sasa kuna haja ya kujenga soko kubwa lenye cold room kwa ajili ya kuhifadhi mazao yale au mbogamboga zile ili wananchi wasiendelee kupata hasara?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; je, Serikali ina mpango gani wa kuwawezesha kwa kuwapelekea wawezeshaji wakulima wa mbogamboga ili kuongeza mnyororo wa thamani katika mazao yetu haya ya mbogamboga na matunda?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Shekilindi, kwa pamoja, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Wilaya ya Lushoto na Wilaya za Mkoa wa Tanga, Serikali sasa hivi inafanya tathmini ya kuangalia maeneo ya kujenga masoko, kwa sababu hatutaki kufanya makosa ambayo yamewahi kutokea huko nyuma katika baadhi ya miradi ambapo hata katika wilaya ya Lushoto, kuna jengo lililojengwa la Ubaridi (cold room facility) ambayo mpaka leo haitumiki. Kwa hiyo, nataka nitumie nafasi hii kumwambia Mheshimiwa Mbunge, hivi sasa tunavyoongea wataalam wa Wizara wako Mkoa wa Tanga wakiangalia wapi tuweke masoko ili tuweze kutatua tatizo la mazao ya mbogamboga na matunda hasa machungwa.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapa pembejeo wakulima wa mbogamboga nchini?

Supplementary Question 2

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Katika Jimbo la Hai kuna wakulima wengi wa mbogamboga wanaolima kwenye mashamba yao binafsi na kwenye vyama vya ushirika, lakini wakulima hao wanaathirika na migogoro iliyopo kwenye vyama vya ushirika. Je, ni lini Serikali itamaliza migogoro kwenye Vyama vya Ushirika Makoa, Mrososangi, Mkundoo, Nkusinde, Byamungo, Narumu na pale Silver Bay ili wakulima hawa waendelee na kazi yao ya kulima?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Saashisha, Mbunge wa Hai, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba kwenye Chama cha Ushirika cha Kikafu chini, Mrososangi, Mkuu, Chama cha Makoa na baadhi ya vyama vingine na hata Chama Kikuu cha KNCU katika Mkoa wa Kilimanjaro kuna migogoro ambayo inaendelea. Nataka nimhakikishie tu kwamba Mrajisi wa Vyama Vikuu vya Ushirika, hivi sasa tumempa ultimatum kwamba kufikia tarehe 30, Mei awe amemaliza migogoro yote iliyopo na wawekezaji ambao wamekuwa chanzo cha migogoro hii katika vyama hivi. Serikali inaendelea kuchukua hatua za kisheria ili tuweze kuwachukulia hatua za kisheria kwa sababu wao kuwa wawekezaji hatuwezi kuwaruhusu waweze kutumia nafasi hiyo kuweza kuathiri vyama vya ushirika na kuruhusu ubadhirifu unaoendelea katika vyama hivi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie tu kwamba Mrajisi wa Vyama Vikuu vya Ushirika anafahamu, kapewa ultimatum na asipochukua hatua za kinidhamu kwa viongozi wa vyama hivi, Serikali itamchukulia yeye hatua na tutamshauri Mheshimiwa Rais amwondoe katika nafasi hii kwa sababu nafasi aliyonayo ni ya uteuzi wa Mheshimiwa Rais.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapa pembejeo wakulima wa mbogamboga nchini?

Supplementary Question 3

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kumekuwa na changamoto sana kwenye suala la masoko hasa katika kilimo cha zao la parachichi na wakulima wamekuwa wakihangaika wenyewe. Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kuna soko la uhakika katika zao hili la parachichi ambalo litaleta Tanzania pesa nyingi za kigeni?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ester, Mbunge wa Viti Maalum na mkulima wa parachichi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni ukweli kwamba parachichi ni moja zao ambalo linakuwa kwa kiwango kikubwa na hivi sasa kama Serikali tuko katika hatua za mwisho tukishirikiana na Wizara ya Viwanda na Biashara kufungua Soko la China ambalo ni soko la uhakika. Vile vile, Waheshimiwa wataona kwamba Serikali imefanya kazi kubwa ya kufungua masoko mengi katika zao la parachichi. Mwaka huu 2023 zao la parachichi export imeongezeka kutoka katika tani 8,000 mpaka tani 29,000. Kwa hiyo, sisi kama Serikali tunaendelea kuchukua hatua.

Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto kubwa ambayo inawakabili wakulima wa parachichi sio soko tu, ni miundombinu ya uhifadhi na miundombinu ya umwagiliaji katika maeneo hayo. Nataka tu niwahakikishie kwenye bajeti mwaka kesho 2024/2025, mtaona mwaka huu 2023/2024 tunaanza kujenga common use facility, lakini mwaka 2024/2025, katika bajeti ya Wizara ya Kilimo kutakuwa na program mpya ya kuwasaidia wakulima 10,000, kuwachimbia visima na kuwapa irrigation kit za Hekta moja kwa kila mtu ili aweze kuweka katika shamba lake. Kwa hiyo Serikali inaendelea kufanya kazi hizo.