Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 16 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 206 2023-05-02

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapa pembejeo wakulima wa mbogamboga nchini?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Shabani Omari Shekilindi, Mbunge wa Lushoto, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika msimu wa 2022/2023, Serikali imeendelea kutekeleza mpango wa utoaji wa ruzuku za viuatilifu, mbegu na mbolea kwa mazao yote yanayozalishwa nchini. Kwa kipekee utekelezaji wa mpango wa ruzuku ya mbolea ni kwa mazao yote ya nafaka, mbogamboga, mikunde na mazao mengine yote yaliyozalishwa na wakulima.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuhakikisha wakulima ndio wananufaika na pembejeo za ruzuku, wanapaswa kujisajili kwa kuainisha mashamba na mazao anayozalisha na hivyo kuweza kununua pembejeo za ruzuku kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na Serikali. Lengo la Serikali kutoa ruzuku za pembejeo kwa mazao yote, ni kupunguza gharama kwa wakulima, kuongeza uzalishaji na tija katika kilimo, kuimarisha usalama wa chakula na kuongeza upatikanaji wa malighafi za viwanda.