Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa fedha za kumalizia ujenzi wa Gereza Chunya?

Supplementary Question 1

MHE. MASACHE N. KASAKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, lakini kiasi cha fedha ambacho kimetengwa takribani Milioni 50 tunashukuru, isipokuwa kiasi hiki ni kidogo sana kuweza kumaliza gereza hili. Swali la kwanza; kwa kuwa Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani bado haijasomwa, je, hatuwezi tukaongeza hizi fedha ili gereza hili liishe kwa wakati?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa gereza hili linakwenda kuisha, sasa ni muda muafaka kuweza kupata vitendea kazi vya ofisi pamoja na gari. Je, Serikali inatuahidi nini ili tuweze kupata vitendea kazi hivyo?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tunatambua ni kiasi kidogo Mheshimiwa Mbunge, lakini tulisema pamoja na ufinyu wa bajeti angalau gereza lile uendelezaji wake usisimame. Hata hivyo, nimuahidi tu kwamba kipaumbele baada ya mwaka huu 2023/2024 mwaka unaofuata 2024/2025, tutaongeza fedha za kutosha ili angalau ujenzi wake uwe wa kasi kubwa zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu umuhimu wa kuwepo vitendea kazi, ofisi tumesema inaendelea kujengwa na gari tutapeleka kutokana na bajeti yetu itakavyoruhusu, ahsante sana.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa fedha za kumalizia ujenzi wa Gereza Chunya?

Supplementary Question 2

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Gereza la Karanga lililopo Mkoani Kilimanjaro ni katika yale magereza ya awali sana Tanzania. Miundombinu yake ni chakavu na hasa nyumba za wafanyakazi. Je, ni lini Serikali itatupa kipaumbele kukarabati gereza hilo?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, Gereza la Karanga tunatambua ni chakavu na ni la muda mrefu, lakini ni gereza ambalo angalau lina miradi ya maana ikiwemo hiki Kiwanda cha Viatu. Jambo moja ambalo namuahidi Mheshimiwa Mbunge, ni kwamba kupitia mapato yao ya ndani ikiwemo ya uuzaji wa viatu, waanze ukarabati lakini ngazi ya Serikali Kuu wataenda kutenga fedha kwa ajili ya kukrabati magereza makongwe ikiwemo Gereza la Karanga kadri bajeti ya Serikali itakavyoruhusu.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa fedha za kumalizia ujenzi wa Gereza Chunya?

Supplementary Question 3

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Gereza la Liwale pamoja na kwamba lina uzio wa miti, Mkuu wa Gereza amejenga nyumba tano za two in One na bado nyumba zile zimeishia kwenye linta. Je, Serikali haioni umuhimu wa kumwongezea fedha Askari yule ili wamalizie nyumba zile za maaskari?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nimuahidi Mheshimiwa Mbunge, kwa wale wanaofanya juhudi kama Mkuu wa Gereza wa Liwale pamoja na juhudi za Mbunge ambaye anatoa fedha kwenye fungu lake kwa ajili ya kuliwezesha gereza hili, tutaendelea kuwa-support kwa kuwapa bajeti ili miradi kama hiyo iweze kukamilishwa ndani ya muda mfupi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.