Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 16 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 205 2023-05-02

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatoa fedha za kumalizia ujenzi wa Gereza Chunya?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Masache Njelu Kasaka Mbunge wa Lupa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa Gereza Chunya ulianza mwaka 2016 kama kambi kwa kujenga na kukamilisha bweni moja la kulala wafungwa, jiko la wafungwa na nyumba mbili za kuishi askari. Vilevile ujenzi uliendelea kwa jengo la utawala na nyumba mbili za kuishi askari ambapo upo kwenye hatua ya msingi. Aidha, katika mpango wa bajeti 2023/2024 Serikali imepanga kutumia kiasi cha shilingi milioni 50 ili kugharamia uendelezaji wa ujenzi wa Gereza Chunya.