Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nicholaus George Ngassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaipatia gari Ofisi ya Zimamoto ya Wilaya ya Igunga?

Supplementary Question 1

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi. Naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mji wa Igunga ni moja ya miji inayokua kwa kasi kubwa sana kutokana na kuongezeka kwa shughuli za kiuchumi na kuongezeka kwa idadi kubwa ya watu.

a) Je, Serikali, kwa kutowapatia mpaka sasa gari la zimamoto haioni ni kuhatarisha maisha ya raia na mali zao endapo itatokea janga la moto?

Mheshimiwa Naibu Spika, mafuta ni moja ya kimiminika hatarishi sana duniani, na sisi Igunga tunashughuli za bomba la mafuta zinaendelea pale na kuna camp kubwa sana ambapo tunaona itakuwa hatari sana endapo shughuli hizi zitaendelea na hatutakuwa na gari la Zimamoto endapo kutatokea na changamoto yoyote ya mlipuko au maafa.

b) Je, Serikali inachukua hatua gani au mkakati gani kwa ajili ya kukabiliana na jambo hili?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika,napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika,kwanza tunatambua kwamba kuna uhaba wa magari ya zimamoto, tumekiri hapa ; na kwamba tumeanza utekelezaji wa bajeti kwa kupunguza tatizo hili kwenye maeneo ambayo hayana, lakini yote yanategemea upatikanaji wa fedha. Hata hivyo, tumesema kwenye jibu la Msingi. Igunga kutokana na hizo shughuli nyingi za kiuchumi pamoja na hilo bomba la mafuta linalopita kwenye eneo lake, tunalipatia kipaumbele kwa mwaka ujao ili wapate gari la kuzimia moto, nashukuru.

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaipatia gari Ofisi ya Zimamoto ya Wilaya ya Igunga?

Supplementary Question 2

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Swali langu, Mkoa wa Njombe na halmashauri mbalimbali nchini ikiwemo Makete wanalipa ushuru wa fire lakini maeneo haya hayana gari za fire. Ni ipi kauli ya Serikali kwa halmashauri zote nchini ambazo haziona gari za fire na wanalipa ushuru wa fire iktu ambacho kwa wnanchi kimekuwa ni kero na wamekuwa wakituuliza maswali mengi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika,ushuru unaolipwa si kwamba ndio unaokwenda kununua gari za zimamoto kwa sababu ni ushuru kidogo sana ukilinganisha na gharama za gari hizi; gharama za gari hizi hutegemea bajeti ya Serikali. Hata hivyo fedha zile zinalipwa kuwezesha Jeshi la Zimamoto na Ukoaji kutoa elimu ya namna ya kujikinga na majanga ya moto na majanga mengine ya kibinadamu kwenye maeneo hayo. Nikuahidi Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wote, kwamba kipaumbele cha Serikali kuanzia mwaka ujao ni kupata fedha ili kuweza kuzipatia wilaya zote gari za zimamoto kwa kadri fedha zitapopatikana, ahsante.

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaipatia gari Ofisi ya Zimamoto ya Wilaya ya Igunga?

Supplementary Question 3

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kunipa nafasi. Mkoa wa Njombe una majanga makubwa sana upande wa misitu, na misitu ndio uchumi. Anaweza kutoa kauli ya Serikali kuhusiana na kutoa kipaumbele kwa mkoa huu muhimu na Mji wa Njombe? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIB WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nimuahidi kwamba itaendelea kutoa kipaumbele kama ambavyo sasa hivi ina gari mbili, moja iko Njombe Mjini nyingine liko Makambako.

Tutaendelea kuimarisha utoaji wa gari hizi ili hatimaye kua- address matatizo ya majanga yakijitokeza katika mkoa huo, nashukuru.

Name

Martha Festo Mariki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaipatia gari Ofisi ya Zimamoto ya Wilaya ya Igunga?

Supplementary Question 4

MHE. MARTHA F. MARIKI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Zaidi ya miaka kumi Mkoa wa Katavi umekuwa hatuna gari la Zimamoto.

Je ni lini Serikali italeta gari la Zimamoto katika Mkoa wa Katavi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika,Mkoa wa Katavi unalo gari moja la zimamoto lakini tunatambua kwamba ni bovu na liko kwenye matengenezo. Tutakachofanya ni kuharakisha matengenezo ya gari hili, ili angalau liweze kurejeshwa Katavi liweze kutoa huduma stahiki, nashukuru.