Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 16 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 204 2023-05-02

Name

Nicholaus George Ngassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaipatia gari Ofisi ya Zimamoto ya Wilaya ya Igunga?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Nicholaus George Ngassa Mbunge wa Igunga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua changamoto ya magari kwa Jeshi la Zimamoto na uokoaji Nchini. Katika mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali imetenga bajeti ya jumla ya shilingi bilioni tatu kwa ajili ya ununuzi wa magari matano ya kuzima moto ambayo yatasambazwa katika mikoa na wilaya zenye upungufu wa magari ya zimamoto na uokoaji nchini ikiwemo Wilaya ya Igunga. Kwa sasa Wilaya ya Igunga inahudumiwa na gari la zimamoto lililopo Mkoani Tabora.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kuliimarisha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwa kuliongezea wataalam na vitendea kazi ikiwemo magari ya kuzimia moto na uokoaji kwa ajili ya kuzifikia wilaya zote nchini kutegemea upatikanaji wa fedha, ahsante.