Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zuena Athumani Bushiri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI aliuliza: - Je, ni lini umeme utafungwa kwenye mnara wa halotel uliopo kata ya Ngujini Wilayani Mwanga?

Supplementary Question 1

MHE. ZUENA A. BUSHIRI: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa katika Wilaya ya Mwanga Mkoani Kilimanjaro kuna kata ambazo hazina mawasiliano mpaka wananchi wapande juu ya miti ndio wapate mawasiliano ; na kata hizo zina changamoto ya kuvamiwa na Tembo mara kwa mara.

a) Je, nini kauli ya Serikali ya kuwasaidia wananchi hao kupata mawasiliano ili wanapopata matatizo waweze kutoa taarifa?

b) Je,ni lini Serikali itadhibiti Wizi wa fedha za wananchi kwa kupitia simu kwa kuwa tatizo hili limekuwa ni changamoto kubwa sana katika nchi hii?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika,napenda kujibu swali la Mheshimiwa Zuwena Athuman Bushiri, Mbunge Viti Maalumu Kilimanjaro kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Zuwena kwa kazi kubwa ya kuwatetea wana Kilimanjaro katika masuala ya mawasiliano. Mheshimiwa Zuwena alifanya Ziara katika Tarafa ya Jipendae, na akatujulisha Serikali na tukapokea malalamiko hayo ambayo ni changamoto, na Serikali tukayafanyia kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kata ambazo Mheshimiwa Zuwena amezitaja, Kata ya Kwakoa, Kilya, Tohora pamoja na kata ya Kibisini tayari zimeingizwa kwenye utaratibu wa kupatiwa huduma za mawasiliano. Lakini katika eneo ambalo linaenda katika lango la Hifadhi ya Mkomazi pia nalo Serikali inatarajia kuingia mkataba na TTCL ili iweze kufikisha huduma ya mawasiliano katika eneo hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwas wali la pili, Serikali haiwezi kupuuza malalamiko ya wananchi. Suala la wizi kwenye masuala ya simu na fedha za wananchi katika mitandao ya simu, nipende kusema jambo moja. Huduma ya mawasiliano ina wadau watatu, kuna watoa huduma, kuna watumiaji wa huduma na kuna Serikali. Serikali kazi yake ni kuhakikisha kwamba watoa huduma wanatoa huduma katika mazingira rafiki, lakini na watumiaji wa huduma wanapata huduma ambayo inaendana na haki ambazo wanazitumia.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kutoa maelekezo kwa TCRA kufanyia kazi malalamiko ya wananchi ili kujiridhisha na changamoto jinsi ambavyo ilivyo na kuhakikisha kwamba tunatoa majibu kwa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI aliuliza: - Je, ni lini umeme utafungwa kwenye mnara wa halotel uliopo kata ya Ngujini Wilayani Mwanga?

Supplementary Question 2

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Ni lini kata ya Mkindi, Kata za Masagaru, Kwekivu na Kimbe vijiji hivi vitapitiwa na minara kwa ajili ya masiliano kwa ajili ya wanachi wa maeneo hayo?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika,napenda kujibu swali la Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mwezi huu wa tano Serikali inatarajia kuingia mkataba na watoa huduma ili kuweza kufikisha huduma ya masiliano katika maeneo 763. Vile vile Serikali imeshaanza kufanya tathmini katika vijiji 2116 vitakavyokamilika. Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kufikisha huduma ya mawasiliano vikiwemo vijiji na kata ambazo Mheshimiwa Mbunge amevitaja, ahsante sana.

Ahsante, Waheshimiwa tunaendelea Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Mheshimiwa Ngasa.