Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO K.n.y. MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapanua barabara ya Tegeta kuelekea kiwanda cha Saruji Wazo?

Supplementary Question 1

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujua sasa barabara ya kutoka Kokoto mpaka Kongowe ni lini upanuzi wake utaanza?

Mheshimiwa Naibu Spika, na swali la pili, Je, ni lini sasa barabara ile ya kutoka Mbande Kisee mpaka Msongora ambayo imekuwa ni adha kwa wapiga kura wa Dar es Salaam ujenzi wake utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze na barabara ya pili Mbande kwenda Msongora kilomita hizo tatu ambazo zimebaki tunategemea zitaanza kutekelezwa katika bajeti hii tunayoanza kuikamilisha. Na barabara hii ya Kokoto kwenda Kongowe upanuzi wake, naomba Mheshimiwa Mbunge asubiri tuone kwenye bajeti tumependekeza tufanye nini. Tunajua tayari kuna changamoto kubwa tuweze kuitekeleza hii barabara.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO K.n.y. MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapanua barabara ya Tegeta kuelekea kiwanda cha Saruji Wazo?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika jimbo la Manyoni Mashariki kuna Barabara ya kutoka Sorya kwenda Hika – Makulu – Londoni na Ikungi Singida.

Je, ni lini Serikali itaanza kufanya upembuzi na usanifu wa kina kwa ajili ya kuijenga katika kiwango cha lami ? Nashukuru.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika,naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hiyo tumeipendekeza ifanyiwe usanifu mwaka wa fedha tunaoanza kama bajeti yetu itapitishwa, ahsante.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO K.n.y. MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapanua barabara ya Tegeta kuelekea kiwanda cha Saruji Wazo?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa barabara yetu ya Kitonga kumekuwa na ajali nyingi sana, na wiki iliyopita tu basi lilitumbukia pale, na ajali ikitokea magari yanakaa takriban siku nzima au siku mbili. Je, lini Serikali itaona sasa umuhimu wa kujenga barabara mbadala ya kutoka Mahenge kwenda Udekwa kupitia Utalisoli mpaka Ilula?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika,ni kweli lile eneo la Kitonga limekuwa na changamoto kubwa. Tayari Serikali ilishatoa maelekezo kwa Meneja wa TANROADS Mkoa wa Iringa wasaidiane na Meneja wa TARURA Mkoa wa Iringa kuangalia uwezekano wa kufanya by-pass ya Mlima Kitonga ili kunapotokea changamoto kuwe na uwezekano wa kuwa na njia mbadala, ahsante.

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO K.n.y. MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapanua barabara ya Tegeta kuelekea kiwanda cha Saruji Wazo?

Supplementary Question 4

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, je, ni lini sasa Serikali itaanza ujenzi wa barabara inayotoka Buza kwenda kuunganisha jimbo la Ukonga pamoja na Temeke?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwa kusaidiana na wenzetu wa TAMISEMI tutahakikisha kwamba hiyo barabara tunaijenga kwa kiwango cha lami.

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO K.n.y. MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapanua barabara ya Tegeta kuelekea kiwanda cha Saruji Wazo?

Supplementary Question 5

MHE. YAHYA A. MHATA: Mheshimiwa Naibu Spika,nashukuru, Mkoa wa Mtwara una unganishwa ni Mkoa wa Lindi hadi Morogoro kwa kuanzia katika Wilaya ya Nanyumbu. Barabara hii iko ndani ya Ilani ya Chama Cha Mapinduzi. Je, ni lini barbara hii itajengwa kwa kiwango cha lami ?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, na kwa kweli tumeongea naye. Hii barabara ni kweli ipo kwenye Ilani. Inapotoka Wilaya ya Nanyumbu kwenda Liwale inapita Selous ambapo inakwenda Ilonga kwenda Mahenge kuunganisha na Mkoa wa Morogoro. Tumeweka kwenye mapendekezo kufanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ili kuunganisha Mkoa wa Mtwara, Lindi na Mkoa wa Morogoro kupitia eneo la Ilonga – Mahenge, ahsante.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO K.n.y. MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapanua barabara ya Tegeta kuelekea kiwanda cha Saruji Wazo?

Supplementary Question 6

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika,ahsante. Je, ni lini Barabara ya Uvinza – Maragarasi yenye kilometa 51 itamalizika kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Uvinza - Maragarasi ni barabara ambayo ipo kwenye ujenzi kwa msaada wa Abu Dhabi na Kuwat Fund, kilometa 51.3 Mkandarasi yuko site. Kinachokwamisha sasa hivi kutokwenda kasi ni kwa sababu ya Mvua nyingi inayonyesha; lakini Mkandarasi ameahidi kwamba atakamilisha kwa muda kulingana na jinsi tulivyokubaliana naye, ahsante.

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO K.n.y. MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapanua barabara ya Tegeta kuelekea kiwanda cha Saruji Wazo?

Supplementary Question 7

MHE. STELLA S. FIYAO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Naoma kujua ni lini Serikali itaona umuhimu wa kujenga barabara ya kutoka Chapwa halmashauri ya Mji wa Tunduma kuelekea Chindi mpaka Chitete ili kurahisisha mawasiliano ndani ya Wilaya ya Momba?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii kwa sasa inahudumiwa na wenzetu wa TARURA, ambayo inaunganisha Makoa Makuu ya Wilaya ya Momba Chitete kuja Tunduma. Hata hivyo nitaichukua ili kama Serikali tuone namna tukavyofanya kuijenga kwa kiwango cha lami ili kuiunganisha Tunduma na Makao Makuu ya Wilaya ya Momba Chitete, ahsante.