Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 16 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 202 2023-05-02

Name

Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO K.n.y. MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapanua barabara ya Tegeta kuelekea kiwanda cha Saruji Wazo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Askofu Josephat Mathias Gwajima, Mbunge wa Kawe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Kipande cha barabara ya Tegeta – Wazo Hill kilikarabatiwa Mwaka 2014 kwa kiwango cha lami kwa njia mbili (Single Carriage Way) ya upana wa mita 7 na njia za waenda kwa miguu zenye upana wa mita 1.5 kila upande. Upana huo unakidhi viwango vinavyohitajika kwa matumizi ya barabara ya njia mbili. Hata hivyo, kutokana na kuongezeka kwa wingi wa magari katika sehemu hii ya Tegeta – Wazo Hill, Serikali ina mpango wa kupanua barabara hii kuwa njia nne na utekelezaji wake utategemea upatikanaji wa fedha.Ahsante.