Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kurudia ujenzi wa Barabara ya Mwigumbi – Maswa ambayo imejengwa chini ya kiwango na imeshaharibika?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza: -

Je, ni kwa kiasi gani Serikali imejiridhisha kuwa marekebisho hayo yamekidhi viwango?

Swali la pili; kwa kuwa barabara ya Kolandoto – Meatu mpaka Kateshi iko kwenye ilani, je, ni lini Serikali itaijenga kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Esther Lukago Midimu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imejiridhisha kwanza kwa kumsimamia zaidi mkandarasi na kuhakikisha kwamba kila hatua anayoifanya mhandisi mshauri pamoja na mkandarasi kupewa majukumu ya kuhakikisha kwamba anakwenda kufanya kazi kwa kiwango kinachotakiwa. Hata hivyo, atakapokuwa amekamilisha kazi hii itahakikiwa na wataalam kuhakikisha kwamba vigezo vyote vya barabara kwa maana ya jinsi ilivyosanifiwa ndivyo ilivyorekebishwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la pili; barabara aliyoitaja ya kuanzia Kolandoto – Meatu kwenda Katesh ni sehemu ya barabara ndefu ambayo ipo kwenye mpango pia wa EPC+F. Ahsante.

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kurudia ujenzi wa Barabara ya Mwigumbi – Maswa ambayo imejengwa chini ya kiwango na imeshaharibika?

Supplementary Question 2

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuweza kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni mwezi mmoja sasa tangu nisimame hapa nikiuliza kuhusu Barabara ya Masasi – Nachingwea, na Mheshimiwa Naibu Waziri utakumbuka ulinijibu kwamba iko kwenye hatua za financing. Na niliuliza lini mchakato huo utakamilika, hatukuweza kupata majibu wakati ule. Sasa ninauliza tena: -

Ujenzi wa Barabara ya Nachingwea – Masasi ambao ulikuwa kwenye hatua ya financing; hatua hiyo itakamilika lini?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii ya Masasi Nachingwea inakwenda mpaka Liwale. Kama nilivyosema, ni kati ya barabara saba ambazo ziko kwenye EPS+F; na taratibu za manunuzi kwa maana ya upande wa finance kwa wenzetu wa fedha bado zinaendelea zote kwa pamoja, kwa barabara zote saba. Kwa hiyo zitakapokuwa mchakato huu umekamilika tutamjulisha Mheshimiwa Mbunge.

Name

Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kurudia ujenzi wa Barabara ya Mwigumbi – Maswa ambayo imejengwa chini ya kiwango na imeshaharibika?

Supplementary Question 3

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Waziri, barabara ya Kibaha – Morogoro -Dodoma kwenda mpaka Mwanza hamuoni kama imelemewa sasa hivi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya kutoka Kibaha hadi Morogoro ipo kwenye PPP ambapo itajengwa kwa express way njia nne; na kutoka Morogoro kuja Dodoma hadi Mwanza ni kweli magari yameongezeka. Serikali ina mpango wa kuipanua hiyo barabara ili iweze kukidhi haja ikiwa ni pamoja na maeneo yote ya miinuko na maeneo ya ku-park kuweza kuipanua ili iweze kukidhi mahitaji ya sasa, ahsante.