Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Joseph Kizito Mhagama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Madaba

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA aliuliza: - Je, kwa nini hoja za ukaguzi hutokea pale fedha za Mfuko wa Jimbo zinapotumika kwa wajasiriamali?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa vile ipo mifuko ya halmashauri ambayo pia inatoa huduma kwenye vikundi vya wajasiriamali na mfuko huu wa maendeleo wa jimbo umeonesha ugumu wa utekelezaji kutokana na masharti yaliyowekwa, kwa nini sasa Serikali isione haja ya kuleta hii sheria ili iboreshwe ili kukidhi mahitaji ya akinamama, vijana na watu wenye ulemavu kama ambavyo wananchi wamekusudia? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Joseph Kizito Mhagama, Mbunge wa Jimbo la Madaba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nimesema kwenye majibu yangu ya msingi, kwamba mfuko huu upo kisheria na ulianzishwa kisheria. Nachukua maoni ya Mheshimiwa Mhagama na tutaona ni namna gani tunakusanya maoni pia kutoka kwa Waheshimiwa Wabunge wengine humu ndani kabla Serikali haijaanza mchakato wa kubadili sheria hii.

Name

Salome Wycliffe Makamba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA aliuliza: - Je, kwa nini hoja za ukaguzi hutokea pale fedha za Mfuko wa Jimbo zinapotumika kwa wajasiriamali?

Supplementary Question 2

MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa kuwa Wabunge wote wa Viti Maalum na Wabunge wa Majimbo wako sawa kwa mujibu wa Katiba. Je, Serikali haioni haja ya kuleta sheria ambayo itaruhusu Wabunge wa Viti Maalum waweze kupewa mfuko wa jimbo ili na wao waweze kushiriki katika maendeleo ya halmashauri? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Salome Wycliffe Makamba, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, pale tutakapoanza kukusanya maoni ya wadau ambao ni ninyi Waheshimiwa Wabunge kwa ajili ya kuona namna gani tunaleta katika Bunge lako hili Tukufu Mabadiliko ya Sheria hii ya Mfuko wa Jimbo, tutazingatia pia hili suala la Wabunge wa Viti Maalum.