Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 16 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 200 2023-05-02

Name

Dr. Joseph Kizito Mhagama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Madaba

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA aliuliza: -

Je, kwa nini hoja za ukaguzi hutokea pale fedha za Mfuko wa Jimbo zinapotumika kwa wajasiriamali?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Joseph Kizito Mhagama, Mbunge wa Jimbo la Madaba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Mfuko wa Kuchochea Maendeleo ya Jimbo ulianzishwa kwa Sheria Na. 16 ya mwaka 2009 na unaelekeza miradi ya kutekelezwa kupitia Kamati ya Mfuko ambayo Mbunge ni mwenyekiti na afisa mipango wa halmashauri ni katibu.

Mheshimiwa Naibu Spika, lengo mahususi la kuanzishwa kwa Mfuko huu wa Kuchochea Maendeleo ya Jimbo ni kutekeleza miradi ya maendeleo iliyoibuliwa katika ngazi ya jamii na kupitishwa kwenye vikao mbalimbali vya kisheria.

Mheshimiwa Naibu Spika, baadhi ya halmashauri zimekuwa zikitumia fedha za Mfuko wa Jimbo kutoa mitaji kwa wananchi, hususan wanawake, watu wenye ulemavu na vijana, hali inayosababisha ugumu wakati wa kufanya ufuatiliaji na tathmini na kusababisha hoja za ukaguzi.