Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Katani Ahmadi Katani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tandahimba

Primary Question

MHE. KATANI A. KATANI aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka fedha kumalizia ujenzi wa sekondari zilizojengwa na wananchi Kata za Mnchimbwe, Kwanyama na Litehu?

Supplementary Question 1

MHE. KATANI A. KATANI: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali: -

Kata za Mahuta na Mkwedu hazina shule ya sekondari kabisa; je, Serikali inaweza ikatupa fedha kwa ajili ya kujenga sekondari hizo kwa sababu tayari wananchi wameshaanza kujenga maeneo yale?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, kata hizi alizozitaja Mheshimiwa Katani hapa Serikali tayari iko mbioni kupeleka shilingi milioni 470 kwenye halmashauri 184 nchi nzima kwa ajili ya ujenzi wa shule nyingine za sekondari katika kata zile ambazo bado hazijapata shule hizi za sekondari. (Makofi)

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KATANI A. KATANI aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka fedha kumalizia ujenzi wa sekondari zilizojengwa na wananchi Kata za Mnchimbwe, Kwanyama na Litehu?

Supplementary Question 2

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Naibu Spika, imekuwa ni utaratibu kwa wananchi kutumia nguvu zao kujenga shule ama zahanati. Lakini bahati mbaya sana kumekuwa kuna udanganyifu kwenye halmashauri, hawazielezei kwa kina thamani ya kifedha ambazo wametumia nguvu za wananchi. Matokeo yake wanaomba Serikali pesa kwa madhumuni kwamba wanataka kumalizia maboma lakini hawaelezi ile nguvu, matokeo yake ni kwamba Serikali inatoa pesa lakini pesa ambayo inatolewa na Serikali haitumiki kwa matumizi yanayotakiwa kwa sababu kuna udanganyifu wa fedha ambayo imetolewa na wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ni lini Serikali itafanya uchunguzi wa kina ili kujua kama fedha zinazotolewa kwa ajili ya kumalizia maboma ni za kumalizia maboma na nguvu za wnanachi vilevile zinajulikana ni kiwango gani?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Halima James Mdee, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekuwa ikifanya tathmini ya mara kwa mara katika halmashauri zetu kuangalia hali ya maboma ambayo yanaripotiwa na wakurugenzi wa halmashauri. Hivi tunavyoongea tayari kuna timu ambayo inafanya tathmini ya kuweza kuona maboma yaliyopo na hizi fedha zinazopelekwa kwenye shule za sekondari na hizi tunazopeleka kwenye shule za msingi kuona wamekwenda kumalizia maboma yaliyokuwepo ama wameanza madarasa mapya. Kwa hiyo Serikali muda wote imekuwa ikifanya tathmini hiyo.