Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 16 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 199 2023-05-02

Name

Katani Ahmadi Katani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tandahimba

Primary Question

MHE. KATANI A. KATANI aliuliza: -

Je, lini Serikali itapeleka fedha kumalizia ujenzi wa sekondari zilizojengwa na wananchi Kata za Mnchimbwe, Kwanyama na Litehu?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI), naomba kujibu swali la Mheshimiwa Katani Ahmadi Katani, Mbunge wa Jimbo la Tandahimba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua jitihada zinazofanywa na wananchi katika kuibua miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa shule. Serikali imeendelea kuunga mkono jitihada hizo kwa kumalizia miradi hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mwaka wa Fedha wa 2020/2021, Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba kupitia mapato ya ndani ilitoa shilingi milioni 200 kwa ajili ya umaliziaji wa Shule ya Sekondari ya Kwanyama. Mwaka wa fedha wa 2021/2022, Serikali illipeleka shilingi milioni 470 kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Sekondari Litehu kupitia mradi wa SEQUIP na Mwaka wa Fedha 2022/2023, shilingi milioni 250 zilitolewa na Serikali kwa ajili ya umaliziaji wa ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Mndumbwe. Aidha, Shule za Sekondari katika Kata za Mnchimbwe, Kwanyama na Litehu zimekamilika, zimesajiliwa na tayari zinatumika.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kutenga fedha za umaliziaji wa maboma ya shule katika halmashauri zote nchini kadri ya upatikanaji wa fedha.