Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Simon Songe Lusengekile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE K.n.y. MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali italipa kiinua mgongo kwa wazee ambao hawajawahi kuajiriwa?

Supplementary Question 1

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, kwa kunipa nafasi kuuliza swali moja la nyongeza. Pamoja na majibu ya Serikali, tunatambua kwamba nchi hii hujengwa na wafanyakazi ambao wameajiriwa na wafanyakazi ambao hawajaajiriwa kwa mfano wakulima na wafugaji.

Je, sasa Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia hawa watu ambao wameijenga nchi yetu kwa muda mrefu wakiwa hawajaajiriwa kwa kazi za Serikali kwa maana ya wakulima na wafugaji ili kuwasaidia wanapofikia umri ambao hawawezi kufanya kazi? (Makofi)

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Simon Songe Lusengekile, Mbunge wa Busega, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Serikali inapaswa kuzingatia Watanzania wote wanaojenga nchi yao katika kufanya kazi mbalimbali. Moja ya mikakati ya Serikali ambayo iliona suala hilo ambalo Mheshimiwa Mbunge amelisema, ni pamoja na kubadilisha skimu za utoaji wa pensheni katika mifuko ya hifadhi ya jamii na kuzingatia kwamba yapo makundi ambayo siyo ya wafanyakazi, wanafanya kazi zisizo rasmi, lakini wanafanya kazi kwa mfano kwenye maeneo ya viwanda, kilimo, biashara na wajasiriamali wadogo wadogo. Tayari Mfuko wa NSSF ambao unashughulika na sekta isiyo rasmi umeanza kukusanya michango kwa kuwatambua hawa walio kwenye makundi mbalimbali.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, bado Serikali pia kwa kutambua kwamba wapo ambao ni wajenzi wa Taifa na wakifikia katika hatua ya uzee wanahitaji msaada. Serikali imekwisha kuandaa vituo vya wazee ambao wanakuwa wanahitaji msaada wa Serikali kwa mfano wa matibabu na maisha, kuna mpango maalum wa TASAF ambapo zaidi ya wazee 647,512 ni wanufaika wa mfuko huo. Lakini zaidi ya hapo pia vipo vituo maalum zaidi ya 14 katika mikoa 26 nchini ambavyo Serikali imeviweka kwa ajili ya kuwasaidia wazee, ahsante sana.

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE K.n.y. MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali italipa kiinua mgongo kwa wazee ambao hawajawahi kuajiriwa?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Kwa kuwa kumekuwa na malalamiko mengi yanayohusu huduma mbalimbali za wazee ikiwemo tiba na mengineyo. Serikali haioni sasa kuna umuhimu wa kuleta Sera ya Wazee Bungeni ili kwa ujumla wake tuangalie mapungufu na yale ambayo yanaweza kufanyika kuweza kujenga mazingira mazuri ya wazee wetu? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Joseph Michael Mkundi, Mbunge wa Ukerewe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze kwa swali zuri ambalo limeendana kabisa na mpango wa Serikali ambao tunaufanya hivi sasa. Katika vituo hivyo vya wazee, na katika utaratibu uleule wa kuangalia makundi ambayo yanahitaji msaada zaidi, hasa katika masuala ya chakula, malazi, mavazi, matibabu na welfare yao kwa ujumla, tayari Sera ya Wazee ipo na iko katika hatua za kwenda kufanyiwa marekebisho ili kuweza kuhakikisha tunawasaidia wazee hawa, ikiwa ni pamoja na kuunda mabaraza ya wazee katika ngazi za halmashauri huko mpaka ngazi ya vitongoji, mitaa na vijiji ambayo tayari imekwisha kuanza kufanya kazi na zinafadhiliwa na halmashauri zetu kote nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.