Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuleta watumishi wa afya na elimu katika Jimbo la Igalula ili kuondoa kero wanayoipata wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. DAUD P. VENANT: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwanza nipongeze Serikali kwa majibu mazuri. Wilaya ya Uyuwi ina upungufu ya watumishi zaidi ya 2,000 lakini pamoja na upungufu huo Serikali imebadilisha utaratibu wa watumishi hasa walimu na madaktari kuwa wakandarasi. Yuko darasani anaambiwa huku mfuko wa simenti umepotea huku anatibu anaambiwa vibarua hawajalipwa.

Je, Serikali haioni haja ya kubadilisha mfumo ili hawa ambao tunao pamoja na upungufu wao wafanye kazi kikamilifu?

Swali la pili, Jimbo la Igaula hatukuwa na shule ya five na six, nashukuru Serikali imetuletea, lakini shule ile ina mchepuo wa sayansi hatuna walimu wa sayansi.

Je, kwenye ajira hizi hauoni unipe upendeleo maalum kwenye ile shule ili iweze kufanya vizuri kwa sababu imeshaanza kufundisha?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa
Spika, swali lake la kwanza hili la nyongeza analo sema kwamba walimu sasa au watumishi kwa ujumla wamegeuka kuwa wakandarasi na kuacha kufanya kazi zao; naomba nimkumbushe Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wengine humu ndani, kwamba wale wakuu wa shule na walimu wakuu ni nafasi za madaraka. Hivyo wao ndio accounting officers katika zile shule zao. Ni kama mtu anapokuwa Katibu Mkuu wa Wizara, anapokuwa Katibu Tawala wa Mkoa, yeye ndiye accounting office. Zile pesa zinaingia kwenye account ya shule husika kwenye mradi. Sasa ni wajibu wao kuhakikisha matumizi ya zile fedha yanakuwa ni mazuri na ya uwajibikaji. Sasa nitolee kwa ujumla kwamba halmashauri bado ina mkono kuhakikisha zile kamati za manunuzi kwenye force account, kamati ya mapokezi na kadhalika zinafanya kazi kwa miongozo na wataalam wa halmashauri kusimamia; lakini bado ni wajibu wa Mkuu wa Shule, ni wajibu wa Mwalimu Mkuu kuhakikisha matumizi ya zile fedha yanakuwa mazuri.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali lake la pili la walimu wa sayansi kupatikana katika hii shule ambayo tayari imeshafanywa kuwa A-level ndani ya halmashauri yake. Nimtoe mashaka Mheshimiwa Mbunge. Ninyi wote ni mashahidi, katika kipindi kifupi cha uongozi wa Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, maeneo yote yamepata watumishi wa kutosha katika kipindi cha miaka hii miwili; na tayari kuna ajira hizi ambazo zimetangazwa. Kwa hiyo nikutoe mashaka Mheshimiwa Mbunge kwamba katika hizi ajira zilizotangazwa tutahakikisha pia na wewe kule katika shule uliyoitaja mnapata walimu.

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuleta watumishi wa afya na elimu katika Jimbo la Igalula ili kuondoa kero wanayoipata wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Spika, ahsante, nilitaka kufahamu ni lini sasa Serikali italeta watumishi wa afya katika Jimbo la Msalala?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, watumishi wa afya kwenda Msalala naamini katika hizi ajira zilizotangazwa sasa ambazo Mheshimiwa Rais ametoa kibali cha kuweza kuajiri watumishi wa afya wa kutosha na Msalala vile vile nanyi mtapata watumishi wa afya.

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuleta watumishi wa afya na elimu katika Jimbo la Igalula ili kuondoa kero wanayoipata wananchi?

Supplementary Question 3

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. halmashauri ya Kyerwa inawatumishi wa kada ya afya 252 ikiwa na mahitaji ya watumishi 1022 ni upungufu wa asilimia 75.

Je, ni lini Serikali itapeleka watumishi wa kutosha kwenye hii halmashauri?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa
Spika, katika ajira hizi ambazo Serikali imetangaza tutahakikisha pia na Halmashauri ya Kyerwa ina pata watumishi wa kwenda kwenye kada ya elimu na kada ya afya vile vile.

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuleta watumishi wa afya na elimu katika Jimbo la Igalula ili kuondoa kero wanayoipata wananchi?

Supplementary Question 4

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Spika, Je, ni lini Serikali itapeleka madaktari kwenye hospitali ya kanda iliyojengwa Mitengo Mkoani Mtwara.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, tutashirikiana na Wizara ambayo ndio wasimamizi wa hospitali hizi za kanda kuhakikisha kwamba Hospitali hii ya Kanda ya Mtwara kule inapata madaktari katika ajira hizi kwa sababu Wizara ya Afya nao wametoa ajira hizi kupitia mfumo wao.

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuleta watumishi wa afya na elimu katika Jimbo la Igalula ili kuondoa kero wanayoipata wananchi?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa kuwa Hospitali ya Manispaa ya Kahama inatibu kama hospitali ya mkoa; ni nini kauli ya Serikali kuhusu kuongeza idadi ya watumishi?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, kwenye ajira hizi ambazo Serikali imetangaza na ambazo mchakato unaendelea tutahakikisha hospitali ya Manispaa ya Kahama nayo inapata watumishi wa kutosha kuweza kusaidia wananchi wa pale Kahama.

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuleta watumishi wa afya na elimu katika Jimbo la Igalula ili kuondoa kero wanayoipata wananchi?

Supplementary Question 6

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Spika, nashukuru, mbali na Serikali kutoa ajira nyingi, Jimbo la Sumve limeendelea kuwa na tatizo la upungufu mkubwa wa watumishi hasa katika sekta ya elimu, kiasi kwamba Shule kama Nyang’enge, Bukala zina walimu kati ya watano mpaka saba.

Je, Serikali haioni sasa umefika wakati wa kutoa upendeleo maalumu katika ajira zinazofuata kwa Jimbo la Sumve ili kukidhi mahitaji ya walimu?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nilikuwa nimeshasema awali kwamba katika kipindi hiki cha miaka miwili ya uongozi wa Doctor Samia Suluhu Hassan, Serikali imejitahidi sana kuhakikisha inaajiri walimu wengi, na ninyi ni mashahidi kwenye halmashauri zenu Waheshimiwa Wabunge mmepata walimu wa kutosha. Kwenye hizi ajira mpya tutahakikisha Sumve pia nanyi mnapata Mheshimiwa Mbunge.