Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 14 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 176 2023-04-27

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuleta watumishi wa afya na elimu katika Jimbo la Igalula ili kuondoa kero wanayoipata wananchi?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI), naomba kujibu swali la Mheshimiwa Daud Protas Venant, Mbunge wa Jimbo la Igalula, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imekuwa ikitoa ajira ili kukabiliana na upungufu wa watumishi katika kada za afya na elimu unaotokana na kustaafu, kuacha kazi, kufukuzwa na kufariki. Tangu mwaka 2018/2019 hadi 2021/2022, Serikali imeajiri jumla ya walimu 26,598 wakiwemo 16,640 wa shule za msingi na 9,958 wa shule za sekondari.

Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2021/2022, watumishi wa kada za afya 7,736 waliajiriwa na kupelekwa kwenye maeneo mbalimbali nchini kulingana na uhitaji uliokuwepo. Mkoa wa Tabora ulipata walimu 565 wakiwemo wa shule za msingi 301 na shule za sekondari 264. Aidha, kwa upande wa kada za afya Serikali ilipeleka kwenye Mkoa wa Tabora jumla ya watumishi 265 ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Uyui ilipata watumishi wa kada ya afya 50.

Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Rais, TAMISEMI tayari imetangaza nafasi za ajira za walimu na watumishi wa kada ya afya kwa mwaka wa fedha 2022/2023. Jumla ya ajira 13,130 kada ya elimu na 8,070 kada ya afya zitatolewa hasa kwa kuzingatia maeneo yenye upungufu mkubwa.