Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maulid Saleh Ali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Welezo

Primary Question

MHE. MAULID SALEH ALI aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kudhibiti utapeli unaofanywa kwa kutumia namba za simu za nje?

Supplementary Question 1

MHE. MAULID SALEH ALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru. Nitakuwa na swali moja la nyongeza.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuimarisha mfumo wa TEHAMA na kudhibiti usalama wa mawasiliano nchini? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Maulid Saleh Ali, Mbunge wa Welezo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Awamu ya Sita inaongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan, tayari imeshatoa mkakati (National Cyber Security Strategy) ya mwaka 2018, mwaka 2023 ambao ni kuhakikisha kwamba kuna usalama katika huduma zote zinazofanyika katika mtandao. Vilevile tunayo timu ambayo inaitwa Mwitikio wa Kukabiliana na Majanga ya Kompyuta (TZ-CERT) ambayo yenyewe kazi yake ni kuhakikisha kwamba pale changamoto kama hizi zinapotokea basi tunahakikisha tunaenda kuchukua hatua ili kuzuia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo jingine tunao mfumo wetu ambao unaitwa Tele Traffic Management System ambao kazi yake ni kuhakikisha kwamba inadhibiti mambo mawili, kwanza kabisa ni kufatilia miendendo ya mawasiliano yote yanayoingia ndani ya nchi, vilevile ni kuangalia namna mapato yanavyotokea na namna ambavyo tunaweza tukaya–contrive.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.

Name

Amina Daud Hassan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAULID SALEH ALI aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kudhibiti utapeli unaofanywa kwa kutumia namba za simu za nje?

Supplementary Question 2

MHE. AMINA DAUD HASSAN: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, utapeli hata hapa kwetu Tanzania unafanyika kwa kuomba michango na kadhalika. Je, Serikali ina mkakati gani wa kushirikiana na TCRA ili kuweza kuwaelewa wahalifu hawa?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA
YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo nimejibu katika swali la msingi. Ni kwamba Serikali ina mkakati maalum na zaidi ya hapo Serikali kwa kushirikiana na Vyombo vya Dola vinaendelea kuratibu na kufatilia mienendo yote ya matumizi ya simu na zile ambazo zinahusika katika utapeli basi huwa zinakamatwa na baadae tunazifungia, sambamba na hilo tunaendelea kutoa elimu kwa Watanzania ili kuelewa pale ambapo simu za namna hii zinapowafikia ili wajue kwamba ni hatua gani waweze kuchukua kwa kuwasiliana na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania - TCRA.

Name

Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAULID SALEH ALI aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kudhibiti utapeli unaofanywa kwa kutumia namba za simu za nje?

Supplementary Question 3

MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na mimi kwa kuniona.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumuuliza Mheshimiwa Waziri, kwamba siyo utapeli wa simu za nje tu lakini pia kuna utapeli wa kiholela wa kuongezewa au kupandishwa vyeo humu nchini. Utapigiwa simu umeambiwa umepandishwa cheo kwa hiyo usubiri barua yako. Kwa hiyo na hili pia linatumika katika njia za simu. Je, Serikali ina mpango gani kuhusu suala hili?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA
YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, utapeli unakuja kwenye picha tofauti tofauti. Kuna picha ya kutafutiwa kazi, picha ya kupandishwa vyeo kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge amesema, lakini sana sana tunachokiomba tu kwa Watanzania ni kwamba pale wanapopokea changamoto kama hizi basi waweze kuwasiliana na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania ili tuweze kuchukua hatua stahiki nasi tukiwa tunaendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi kupitia kitengo chao cha Cyber Crimes Act. Kwa hiyo, tunaamini kabisa kwa ushirikiano huu basi tutaweza kuhakikisha kwamba changamoto hizi zinadhibitiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vita dhidi ya matapeli siyo vita dhidi ya Serikali peke yake, ni vita dhidi ya umma na kwa pamoja tukifanya kazi kwa pamoja tutahakikisha kweli tumetokomeza changamoto kama hii. Nakushukuru sana.

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. MAULID SALEH ALI aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kudhibiti utapeli unaofanywa kwa kutumia namba za simu za nje?

Supplementary Question 4

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Je, Serikali inachukua hatua gani kwa matapeli wanaotumia lane za ndani ambazo zimesajiliwa?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA
YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesema tuna mfumo unaoitwa Tele Traffic Management System, kwanza kabisa tunabaini simu ambazo zinafanya mambo ambayo hayastahiki na mpaka sasa tunatumia mfumo huo ambao unatumia simu za majaribio (Test Calls) na tukitumia baadae tunabaini na tangu Julai mwaka 2022 mpaka sasa ni takribani simu 826,951 zilibainika kufanya mambo ambayo yasiyostahili lakini kati ya hizo tayari tumeshachukua hatua na bahati mbaya sana tunapochukua hatua katika mambo haya huwa hatuyatangazi kwa sababu tunakuwa tumepeleka kwenye mamlaka ambayo yanatakiwa kutoa hukumu na katika mchakato huo bado kunakuwa na ukusanyaji wa taarifa na evidences ambazo zitafanya kwamba hukumu iweze kutoka vizuri, ndiyo maana huwa hatutangazi lakini Serikali imejizatiti kuhakikisha kwamba jambo hili linaendelea kukomeshwa, ahsante sana.

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAULID SALEH ALI aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kudhibiti utapeli unaofanywa kwa kutumia namba za simu za nje?

Supplementary Question 5

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Serikali ilianzisha mfumo wa usajili wa biometric tukawa tunatumia vile vile finger prints kwa lugha nyingine ili kuweza kuwa–track ama kuwe na database ya kila mtu ambaye ana namba ya simu. Lakini ukweli ni kwamba watu wanatapeliwa kwa namba za simu ambazo zimesajiliwa. Sasa swali kwenu Serikali, unataka kukiri mbele yetu kwamba wizi wa kwenye mitandao ya simu unafanyika kwa makusudi baina ya makampuni ya simu na matapeli na mfumo wa Serikali?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA
YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Halima Mdee, Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo nimesema, changamoto ya utapeli kwanza kabisa ni jukumu letu sisi sote kushirikiana, lakini Serikali tunaendelea kutoa elimu kwa umma ili waweze kujua namna ya kujidhatiti na kupambana na changamoto kama hii. Pamoja na hivyo Serikali sasa imeendelea kuwekeza Zaidi katika mifumo ya TEHAMA ili iweze kudhibiti katika picha ya ki–technical zaidi kuhakikisha kwamba mambo haya yanaendelea kupungua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ki ukweli hasa kipindi cha pandemic, mambo kama haya ndiyo yanakuwa mengi zaidi, kwa sababu mawasiliano yanakuwa siyo ya moja kwa moja, simu ndiyo zinakuwa medium of communication. Kwa hiyo, tunaamini kabisa kwa kuimarisha mifumo ya TEHAMA tutaendelea kuhakikisha kwamba changamoto hii inaendelea kupungua katika Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. (Makofi)