Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YUSTINA A. RAHHI aliuliza: - Je, ni lini Serikali italeta Bungeni Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 kuhusu Ndoa za Utotoni?

Supplementary Question 1

MHE. YUSTINA A. RAHHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana na naishukuru Serikali tunategemea kuletewa Muswada, lakini nina maswali madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; sheria hizi zinazohusu ukiukwaji wa haki za kibinadamu ikiwepo ndoa za utotoni, ukeketaji, ubakaji, ulawiti, ukatili wa kijinsia pamoja na kutungiwa sheria kali ikiwepo miaka thelathini jela kwa kosa la ubakaji, lakini matendo haya yamekuwa yakiongezeka kwa kasi kubwa. Sababu kubwa ni kutoa mwanya wa makosa hayo kusuluhishwa kijamii. Je, sasa Serikali inasimamiaje sheria hizi kuhakikisha kwamba inaondoa ukiukwaji wa haki za kibinadamu? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili; Sheria ya Ndoa inasemaje kuhusu wanawake kumiliki mali? Ahsante sana.

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa nafasi nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Rahhi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge ameeleza vyema kwamba tatizo siyo sheria, tatizo ni sisi wanajamii kutokuwafikisha hao wahalifu kwenye vyombo vya dola. Nitoe rai kwa wanajamii kwamba makosa haya yanaumiza Watanzania wenzetu, Watoto, wasiyavumilie kwa kuyasuluhisha nyumbani na kuisha, wapeleke kwenye vyombo vinavyohusika hatua zichukuliwe kwa mujibu wa sheria kama ambavyo sheria zetu zinataka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili Mheshimiwa Mbunge amehitaji kufahamu Sheria yetu ya Ndoa inasemaje katika umiliki wa mali. Sheria hii ya Ndoa siyo kwamba ni mbaya kiasi hiki ambavyo watu wanafikiria, ina vifungu zaidi ya 167, ni vizuri kabisa, vichache tu ndiyo vina usumbufu Kifungu cha 13 na 17. Sheria yetu hii imesema katika Kifungu kile cha 56 wanandoa wote wana haki ya kumiliki mali, iwe ni mke iwe ni mume wote wana haki sawa. (Makofi)

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. YUSTINA A. RAHHI aliuliza: - Je, ni lini Serikali italeta Bungeni Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 kuhusu Ndoa za Utotoni?

Supplementary Question 2

MHE. NOAH L. S. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuuliza swali la nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Mahakama ilishatoa uamuzi kuhusu suala la umri la watoto wadogo kuolewa Tanzania. Serikali haioni kuendelea kukusanya maoni ni kukiuka amri ya Mahakama?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kunipa nafasi nijibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali na Mheshimiwa Waziri wa Katiba na Sheria amesema vizuri kwamba, tulishaleta kwenye Bunge lako hili Tukufu na nimesema kwenye majibu yetu ya msingi, kwamba ni Bunge hili na Kamati hii ilitutaka turudi kwa wananchi ili tupate wigo mpana wa kuwahusisha Watanzania katika hili. Kwa sisi hatuna tatizo na niwakaribishe Waheshimiwa Wabunge kesho wenye nafasi mje tunamaliza hayo majadiliano katika Hoteli ya Morena kesho Saa Saba Mchana, tukishakamilisha tutaleta sheria hii Bungeni. Ilikuwa ni agizo la Bunge siyo la kwetu.

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YUSTINA A. RAHHI aliuliza: - Je, ni lini Serikali italeta Bungeni Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 kuhusu Ndoa za Utotoni?

Supplementary Question 3

MHE. NUSRAT S. HANJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na utayari wa Serikali kufanya marekebisho ya Sheria ya Ndoa lakini bado kuna Sheria za Kimila kandamizi kwenye mirathi. Je, ni kwa nini sasa Serikali isione haja ya kupitia upya Sheria za Kimila ili kuondoa ukatili wa kijinsia na ukandamizaji wa wanawake? (Makofi)

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kunipa nafasi nijibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Nusrat, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni sahihi kwamba sheria zetu za kimila, tuna sheria tatu za mirathi, tuna ya kidini Sheria ya Kiislamu Sheria ya Kimila na Indian Succession Act. Hizi sheria zote zimekuwa zikizungumzia jinsi gani watu wananweza kupata haki zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, miongoni mwa sheria ambazo tumezisema katika Bunge hili kwamba tunazifanyia marekebisho ni pamoja na sheria hizi za mirathi za kimila ili Watanzania wote wapate haki zao. Kwa sababu katika sheria ambayo Mheshimiwa Mbunge ame-refer wanawake wengi hawapati haki zao, wanakuwa katika marriage lakini watoto wanapewa mali wakati wale akina mama ambao wamezaa wale watoto wanakosa haki. Kwa hiyo, tunakuja na marekebisho ya sheria hizo. (Makofi)