Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 13 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 173 2023-04-25

Name

Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YUSTINA A. RAHHI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali italeta Bungeni Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 kuhusu Ndoa za Utotoni?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria naomba kujibu swali la Mheshimiwa Yustina Arcadius Rahhi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ikumbukwe kuwa Muswada wa Sheria ya Ndoa ulifikishwa kwenye Kamati ya Bunge lako Mwezi Februari, 2021, kufuatia maamuzi ya Mahakama ya Rufani kati kesi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali dhidi ya Rebecca Gyumi, Rufaa Na.204/2017 iliyotokana na kesi Na.5/2016 ya Mahakama Kuu iliyotaka Sheria ya Ndoa ifanyiwe marekebisho ili umri wa mtoto kuingia katika ndoa iwe kuanzia miaka 18. Kamati ya Bunge baada ya kupitia iliona upo uhitaji wa kushirikisha wadau wengi zaidi ili kupata maoni zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nipende kumwarifu Mbunge kuwa Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imeshakusanya maoni kutoka kwa wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa kidini, viongozi wa kimila, viongozi wa vyama vya siasa, wanafunzi, wataalam mbalimbali wa afya, makundi mbalimbali ya wananchi wakiwemo watu wenye ulemavu. Aidha, tarehe 26 Aprili, 2023, Wizara imeandaa Kongamano la Sheria ya Ndoa litakalofanyika katika Hotel ya Morena, Jijini Dodoma, kesho saa saba. Naomba niwakaribishe Wabunge wote na itakuwa live TBC kwa Watanzania wote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mara tu baada ya Serikali kukamilisha zoezi hili la mwisho, inatarajia kuwasilisha Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Ndoa Bungeni katika Bunge hili la Bajeti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.