Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA K.n.y. MHE. TAUHIDA CASSIAN GALLOS aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kukusanya madeni ya TANESCO katika taasisi kubwa ili shirika hilo liweze kujiendesha?

Supplementary Question 1

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niulize maswali mawili ya nyongeza kwa niaba ya Mheshimiwa Tauhida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; kwa kuwa mpango huu wa Serikali umekuwepo kwa siku kidogo lakini bado ulipaji wa madeni umesuasua. Je, ni mikakati gani ya dharura ambayo Serikali itachukua kuhakikisha kwamba ulipaji unafanyika kwa uharaka na kwa ufanisi zaidi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa bilioni 244 ni pesa nyingi sana inazodai Serikali, je, Serikali ina mikakati gani ya kisheria ambayo itachukua kuhakikisha kwamba hizi pesa zinalipwa kwa kuwapeleka hawa watu Mahakamani au kwa njia nyingine yeyote, lakini pesa hizi zilipwe ambazo ni muhimu sana kwa maendeleo ya shirika na nchi yetu kwa jumla?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Asha Abdullah Juma kwa pamoja, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niseme hizi pesa bilioni
244 kwa sehemu kubwa ni deni la nyuma na ni deni la siku nyingi. Ni deni ambalo lilikuwepo kipindi kile ambacho bado tulikuwa hatujaanza kutumia LUKU na tulikuwa hatujaweza kukusanya vizuri. Kwa hiyo ni madeni ya siku nyingi na tunaendelea kuhangaika nayo kama ambavyo Mheshimiwa amesema tuna mkakati gani wa kuhakikisha kwamba tunayakusanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa mikakati iliyopo ya kukusanya pesa hizi kwanza ya dharura kabisa tayari TANESCO imeshakamilisha taratibu za kuwapata madalali wa kukusanya madeni wawili ambao taratibu zinakamilishwa na siku siyo nyingi wataanza kuingia mtaani na kukusanya fedha hizi ambazo ziko kwa watu mbalimbali ili kuweza kuzipata.

Mheshimiwa Mwenyekiti, cha pili upande wa Serikali, Wizara na TANESCO tumeshirikiana na kuiomba Serikali kupitia Hazina ilipe pesa hii yote inayodaiwa kwa TANESCO ili TANESCO iweze kupata fedha ya kuweza kujiendesha. Sasa kwenye mikakati inayokuja ya nini kinafanyika pamoja na hizi LUKU ambazo tumeshaweka, lakini zinawekwa LUKU zinaitwa boundaries meters ambazo zitawekwa kwenye ngazi ya Mkoa ili kila Mkoa tujue inatumia umeme kiasi gani. Pia tunakwenda kwenye kuweka smart meters ambazo zitatusaidia kujua mtu anapogusa meter yetu moja kwa moja tukiwa ofisini tutaiona na kuhakikisha kwamba tunashughulikia suala hilo mara moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Mahakama, tusingependa tufike huko mapema kwa sababu Mahakama inachukua muda mrefu na process nyingi, lakini wale wateja ambao tunashindwana kabisa hata zile hatua za kukata umeme, basi tunapelekana Mahakamani. Zipo kesi kadhaa ambazo tumeenda Mahakamani na tumeshinda na tuna uhakika kwamba deni hili tutalikusanya lote ndani ya muda mfupi.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA K.n.y. MHE. TAUHIDA CASSIAN GALLOS aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kukusanya madeni ya TANESCO katika taasisi kubwa ili shirika hilo liweze kujiendesha?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Taasisi ambazo zinaongoza kudaiwa deni na TANESCO ni Taasisi za Serikali tena zile andamizi, za binafsi either hamna kabisa au ni moja, mbili au tatu, nataka kujua sasa kwa sababu kuna Taasisi zingine zinatoa huduma kwa wananchi, haziwezi kukatiwa umeme. Je, ni kwa nini Serikali isiweke pre- paid meter kwa hizi Taasisi zote ili ziweze kuwajibika na kuona kipaumbele cha kwanza cha ku–fine kuweza kulipia umeme kuliko hivi sasa kuweza kuleta usawa kati ya wananchi na hizi Taasisi? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye hii bilioni 244 Serikali inadaiwa kama bilioni 86 hivi kwa hiyo bilioni mia moja ishirini na kitu zinazobakia wateja binafsi na watu mbalimbali ndiyo wanaodaiwa. Hao wateja binafsi ni wale wateja wadogo wadogo na kama nilivyotangulia kusema, madeni haya hasa ni ya kipindi kile ambapo hatukuwa na meter.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kwa utaratibu tunaokwenda nao tumeshaongea na wenzetu Serikalini kukubaliana kwamba pesa inayolipwa kwenye zile taasisi kwa ajili ya kulipia huduma ya umeme, hii ya deni ikatwe at source kwa maana ya kutoka Hazina, lakini hizi pesa nyingine zinazokuja basi tuweke utaratibu mzuri ambazo tutaweza kuzikusanya. Pre paid meters na na hizo smart meters zinazokuja tutahakikisha tunazi–roll kwenye maeneo yote ili kila mmoja aweze kuwa na wajibu wa kulipa deni lake kwa wakati tukihakikisha kwamba sasa ni kwa manufaa yetu sisi wazalishaji na watumiaji wa umeme tunaozalisha.