Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 13 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 172 2023-04-25

Name

Tauhida Cassian Gallos Nyimbo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA K.n.y. MHE. TAUHIDA CASSIAN GALLOS aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kukusanya madeni ya TANESCO katika taasisi kubwa ili shirika hilo liweze kujiendesha?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri napenda kujibu swali la Mheshimiwa Tauhida Cassian Gallos, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mpaka kufikia mwezi Machi, 2023, TANESCO inadai jumla ya shilingi bilioni 244 kutoka kwa wateja wake mbalimbali wakiwemo wateja wa umma na wateja binafsi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuzuia ukuaji na kuwezesha ukusanyaji wa deni, kwa upande wa Serikali, Serikali inahakikisha inatenga na kuweka fungu la fedha za kulipia huduma hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, TANESCO imeweka mikakati ya kukusanya na kuzuia madeni kwa kuweka mita za LUKU, kuhamasisha na kufuatilia madeni na inapobidi basi kukata huduma ya umeme kwa mteja mwenye deni kubwa na sugu ili liweze kulipwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.