Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatangaza kumbukizi za Vita vya Majimaji vilivyoanzia Kijiji cha Nandete katika Gazeti la Serikali?

Supplementary Question 1

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Tangu mwanzo wakati Mheshimiwa Waziri, anatoa jibu nimeonyesha masikitiko makubwa sana kwa swali langu kutojibiwa, lakini nimshukuru Mheshimiwa Waziri, katika paragraph ya mwisho ya swali lake ameeleza ukweli kwamba swali hili lilipaswa kujibiwa na Wizara ya Maliasili na Utalii, tena ametaja mpaka sheria ambayo inaipa Mamlaka Wizara ya Maliasili na Utalii, kutangaza hizi kumbukumbu za kihistoria kwenye Gazeti la Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nikiombe kiti chako kwa kuwa swali halikujibiwa. Siku ya Ijumaa tarehe 28, saa tatu asubuhi niiombe Wizara ya Maliasili na Utalii, iweze kuja kujibu swali hili kwa ufasaha. (Makofi)

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu mchango wa Mheshimiwa Francis Ndulane, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali tunafanya kazi kwa kuwajibika kama Serikali moja na ndiyo maana nimemjibu Mheshimiwa Francis Ndulane kwamba pamoja na swali kuja Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa nikaelezea sheria ambayo inatuongoza. Kwa hiyo nimwondoe wasiwasi tutashirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii, kuhakikisha tunashirikiana na Mheshimiwa Mbunge kumwongoza na kupitia utaratibu ambao nimeueleza wa kuangalia hiki Kijiji cha Nandete kama kina sifa ya kuingia kwenye kumbukumbu za nchi yetu za maeneo ambayo yalitumika katika vita vya maji maji, ahsante sana.

Name

Tecla Mohamedi Ungele

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatangaza kumbukizi za Vita vya Majimaji vilivyoanzia Kijiji cha Nandete katika Gazeti la Serikali?

Supplementary Question 2

MHE. TECLA M. UNGELE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa maeneo mengi Mikoa ya Lindi na Mtwara yalihusika katika harakati za Ukombozi wa Bara la Afrika hasa Kusini mwa Bara la Afrika.

Je, Serikali ina mpango gani kuharakisha maendeleo katika maeneo hayo ambayo yaliathirika? (Makofi)

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mama yangu Tecla, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, cha kwanza kabisa mchango wa wapigania uhuru kwa ajili ya nchi yetu kupata Uhuru kutoka kwa Mkoloni fidia yake haipimiki. Kwa sababu mashujaa hawa walijitoa kwa ajili ya nchi yetu kupata uhuru na tunajifunza kutoka kwao kwamba uzalendo huu lazima tuuendeleze na tuwe tayari kupigania nchi yetu bila kutegemea fidia, lakini vile vile nimwondoe wasiwasi Mheshimiwa Mama yangu, Mheshimiwa Tecla, Serikali ya Chama cha Mapinduzi katika kutekeleza Ilani inapeleka maendeleo kote nchini ikiwemo maeneo ya Mikoa ya Kusini. Kwa hiyo ningependa kumwondoa wasiwasi Mipango ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi iko makini katika kuhakikisha maendeleo tunayapeleka kote ikiwemo maeneo ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyataja. (Makofi)