Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 13 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 171 2023-04-25

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatangaza kumbukizi za Vita vya Majimaji vilivyoanzia Kijiji cha Nandete katika Gazeti la Serikali?

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Francis Kumba Ndulane, Mbunge wa Jimbo la Kilwa Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Vita ya Maji Maji ilipiganwa kuanzia Mwaka 1905 hadi 1907, kusini mwa nchi yetu katika baadhi ya Mikoa ya Lindi, Iringa, Morogoro na Ruvuma, ikiwa
na lengo la kupinga utawala na ukandamizaji wa ukoloni wa Mjerumani. Mwaka 2006, Makumbusho ya Taifa ilianza kuadhimisha kumbukizi ya miaka 100 ya Vita ya Maji Maji na inaendelea kuadhimishwa tarehe 26 Februari kila mwaka, katika Manispaa ya Songea kwenye eneo la Makumbusho ya Vita vya Maji Maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, huadhimisha siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa tarehe 25 Julai kila mwaka, ili kuwaenzi mashujaa wetu waliopoteza maisha katika vita na operesheni mbalimbali za ukombozi wa nchi yetu na Bara la Afrika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mamlaka ya kutangaza eneo lolote au lengo la kihistoria iko chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Idara ya Mambo ya Kale, chini ya Kifungu cha Sheria ya Mambo ya Kale, Sura ya 333 ya Mwaka 2002, kifungu cha 3(1) na (2). Sheria hiyo inampa mamlaka Waziri mwenye dhamana ya Malikale kutangaza eneo lenye sifa ya Urithi wa Taifa kwenye Gazeti la Serikali. Endapo Mheshimiwa Mbunge ana nia ya Kijiji cha Nandete kutangazwa katika Gazeti la Serikali kwa ajili ya Kumbikizi ya Vita vya Maji Maji, basi namshauri awasilishe ombi hilo Wizara husika ili liweze kufanyiwa kazi, ahsante sana.