Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA (K.n.y. MHE. HAWA S. MWAIFUNGA) aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwalinda watoto walio tayari kwenye ndoa wakiwa na umri mdogo?

Supplementary Question 1

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri pamoja na kutaka kuwasaidia watoto hawa wa kike lakini mahakama ilisema sheria ya ndoa ibadilishwe;

Je, ni lini Serikali mtaanza kutekeleza sheria hiyo na kubadilisha ili tusiwe na watoto wengi ambao wanaozeshwa wakiwa na umri mdogo?

Name

Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, ninaomba kujibu swali la kwanza la Mheshimiwa Sophia Mwakagenda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tayari Serikali ilitoa maelekezo katika Bunge lako Tukufu, kwamba mchakato wa kukusanya maoni kwa ajili ya kurekebisha sheria ya ndoa umekamilika, na kwamba tarehe 26 Aprili, yaani kesho, kutakuwa na kongamano la mwisho kupitia maoni hayo na baada ya hapo Serikali italeta muswada huo Bungeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha. (Makofi)

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA (K.n.y. MHE. HAWA S. MWAIFUNGA) aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwalinda watoto walio tayari kwenye ndoa wakiwa na umri mdogo?

Supplementary Question 2

MHE: SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, umezungumzia suala la kusaidia program nyingi zinazoendelea mikoani. Ni kweli mmeweka ada ndogo nyingine hadi shilingi 10,000 lakini mahitaji ya wasichana hawa kwenda kusoma ni zaidi ya 400,000; kwamba, aje na godoro na mambo mengine mengi, hamuoni kwamba mnawaonea wasichana wa vijijini na wanakosa haki ya kuweza kuhudhuria mafunzo hayo?

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la pili la Mheshimiwa Hawa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inafanya jitihada mbalimbali ya kuwapa mafunzo walengwa kwa kuwakwamua mabinti wenye mahitaji maalum ikiwa ni pamoja na kuwafikia katika vijiji vyao ili kuondokana na madhila na kujikwamua kiuchumi ili waweze kuimarika na shughuli mbalimbali za kiuchumi. Pia hadi kufikia Februari, 2023, jumla ya vikundi 6,127 vya wanawake, vijana na wenye ulemavu wameunganishwa na kupewa mikopo midogo midogo ambayo inawawezesha kuwainua kiuchumi ili waondokane na mashaka ya kiuchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameelekeza asilimia 10 za Miradi ya Maendeleo zipelekwe katika mifumo ya kibenki kuwakwamua wananchi wote ili waweze kupata fedha hizo kwa ajili ya kujijengea uchumi na kuimarisha uchumi wao kwa maendeleo ya maisha yao, ahsante. (Makofi)

Name

Salome Wycliffe Makamba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA (K.n.y. MHE. HAWA S. MWAIFUNGA) aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwalinda watoto walio tayari kwenye ndoa wakiwa na umri mdogo?

Supplementary Question 3

MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi kuuliza swali dogo la nyongeza. Kiutaratibu Mahakama inapokuwa imetoa maelekezo kwenye jambo hili la watoto wa kike kuolewa chini ya umri, Mahakama ilishatoa maamuzi kwamba Serikali ilete mabadiliko ya sheria Bungeni.

Swali langu, Serikali imepata wapi nguvu ya kukiuka maamuzi ya Mahakama ya kuleta Muswada wa Sheria Bungeni na badala yake inakwenda kukusanya maoni ya wadau kuhusiana na sheria hii? (Makofi)

Name

Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Salome Wycliffe Makamba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya Mahakama ya Rufani kutoa maamuzi ya mwisho kuhusiana na jambo hili, Serikali ilileta Muswada hapa Bungeni. Muswada huo ulipokelewa na kwa maelekezo ya Bunge lako tukufu tulielekezwa na Bunge tukakusanye maoni zaidi. Kwa hiyo ilichokifanya Serikali ni maelekezo ya Bunge, otherwise Serikali ilishaleta Muswada hapa. Tumetekeleza hayo maelekezo ya Bunge na tuko tayari kurudi tena kupokea maoni mengine ya Bunge itakavyoona inafaa. (Makofi)

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA (K.n.y. MHE. HAWA S. MWAIFUNGA) aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwalinda watoto walio tayari kwenye ndoa wakiwa na umri mdogo?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Ubakaji na ulawiti kwa watoto ni zaidi ya uuaji. Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kuondoa dhamana kwa wale wanaume wanaolawiti na kubaka watoto? (Makofi)

Name

Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Thea Ntara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania dhamana ni haki ya mtuhumiwa na inaweza ikaondolewa tu pale ambapo inaonekana ni muhimu na mazingira yanalazimisha lazima iondelewe. Katika kesi nyingine zote hizi discretion ya kuondoa dhamana inabakia kwa Mahakama, endapo Mahakama itaridhika kwenye mazingira haya, huyu mtu asipate dhamana, basi hatapata dhamana hata kesi hizo za ulawiti na ubakaji kama ambavyo Mheshimiwa ameuliza. (Makofi)