Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: - Je, lini ujenzi wa kivuko cha waenda kwa miguu katika eneo la Kisimani barabara kuu itokayo Custom kwenda Sumbawanga itaanza?

Supplementary Question 1

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nishukuru majibu mazuri ya Serikali, lakini kwa kuwa kukosekana kwa hicho kivuko kumekuwa kunatokea ajali za mara kwa mara. Kwanza kwa wananchi vilevile kwa bajaji pamoja na magari. Sasa nilitaka nifahamu kwamba kwa nini Serikali isione kwamba kuna umuhimu mkubwa sana wa kuharakisha upatikanaji wa hizo fedha ili hicho kivuko kiweze kujengwa ili kuwapunguzia adha kubwa wanayopata wananchi wa Mji wa Tunduma; vilevile ikizingatiwa kwamba ilikuwa ni ahadi ya Rais wa Awamu ya Tano?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Juliana Daniel Shonza Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimwakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba eneo analolisema na changamoto anayoisema mimi binafsi ninaifahamu na ni sehemu ambayo na mimi barabara hii naitumia sana. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwamba jitihada zimeshaanza kuchukuliwa kuweka hizo alama za kusaidia kupunguza ajali.

Mpango wa Serikali kwa sasa tayari wanafanya usanifu kuangalia namna ya kuweka kivuko cha chini badala ya kivuko cha juu kwa sababu tumekuja kuona kwamba mara nyingi vivuko vya juu havitumiki sana kuliko vivuko vya chini.

Kwa hiyo nimwakikishie Mheshimiwa Mbunge, Serikali inatambua na iko tayari kuwalinda wananchi na kivuko hicho kitajengwa kama kilivyoahidiwa na Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano, ahsante.

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: - Je, lini ujenzi wa kivuko cha waenda kwa miguu katika eneo la Kisimani barabara kuu itokayo Custom kwenda Sumbawanga itaanza?

Supplementary Question 2

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, natoa pole kwa wananchi wetu wa Halmashauri ya Mji wa Ifakara kwa mafuriko makubwa ambayo wameyapata, na tunashukuru Mungu mpaka sasa hakuna kifo kilichotokea, tunapambana kupeleka misaada kwa wananchi ambao wameathirika sana. Mafuriko haya yamethibitisha kwamba kuna miundombinu ya TANROADS katika Kalavati la Sheli ya Madinga kwenda Rumomo na Kalavati la Kwa Shungu kwamba ni madogo na ndio yalichangia kupatikana kwa mafuriko.

Je, Serikali ina hatua gani za haraka za kurekebisha makalavati haya kama tulivyotembea na Mheshimiwa wa Wilaya na kujionea?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante naomba nitumie nafasi hii kumwagiza Meneja wa Mkoa wa Morogoro aende hilo eneo ambalo makalavati ni madogo atafute namna ambavyo anaweza akaongeza hayo makalavati kwa haraka ili kuondoa changamoto ambayo inawakuta wananchi wa Jimbo la Kilombero kwa Mheshimiwa Asenga, ahsante.