Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 13 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 169 2023-04-25

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: -

Je, lini ujenzi wa kivuko cha waenda kwa miguu katika eneo la Kisimani barabara kuu itokayo Custom kwenda Sumbawanga itaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Juliana Daniel Shonza Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Katika eneo la Kisimani lililoko kwenye Barabara ya Tunduma kwenda Sumbawanga, kumewekwa alama za kuvuka (Pundamilia – Zebra Crossings) na Taa za kuongoza magari na watembea kwa miguu zimewekwa sehemu mbili; ya kwanza mita 300 kutoka eneo la Kisimani na ya pili mita 500 kutoka taa za kwanza za kuongozea magari na watembea kwa miguu (Traffic Signals). Aidha, Serikali ina mpango wa kujenga kivuko cha chini (underpass) katika eneo la Kisimani na utekelezaji wake unategemea upatikanaji wa fedha ahsante.