Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. FESTO R. SANGA aliuliza: - Je, ni hatua gani ya upembuzi yakinifu wa barabara ya Chimala – Matamba hadi Kitulo imefikiwa na lini ujenzi utaanza?

Supplementary Question 1

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, kwa niaba ya wananchi wa Makete nipende kuishukuru Serikali kwa kuichukua barabara hii ya kutoka Chimala kuelekea Matamba kilomita 20 ambayo ina kona 53 kwenye milima. Barabara hii ni ya kiuchumi na barabara ya kimkakati, kwenda TANROADS ni msaada mkubwa ambao Serikali imeweza kutusaidia.

Je, kwa kipindi hiki ambacho mvua nyingi zinaendelea Matamba na Makete ni upi mpango wa Serikali kutusaidia barabara hii iweze kupitika kwa sababu wananchi wanaitumia sana kwa muda mwingi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kuna barabara kutoka Kitulo kuelekea Busokelo kwa Mheshimiwa Naibu Waziri wa Uchukuzi, upi mkakati wa Serikali kuimalizia barabara hii ili iweze kujengwa irahisishe mawasiliano kati ya wananchi wa Makete na wananchi wa Jimbo la Busokelo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Festo Richard Sanga Mbunge wa Makete kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la Matamba hadi Kitulo ni eneo ambalo kwa kweli Mheshimiwa Mbunge atakubaliana na mimi lina mvua nyingi sana, na TANROADS wako barabarani kuhakikisha kwamba inapitika lakini yako maeneo ambayo tunashindwa kufanya kazi kwa sababu ya mvua nyingi sana ambayo inaendelea kunyesha. Hivi tumewaagiza TANROADS kuhakikisha kwamba muda mwingi wawepo maeneo hayo ili pale ambapo jua linatoka basi waweze kuhakikisha kwamba wananchi wanapata mawasilano na kurekebisha zile barabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na kwa swali lake la pili, kuhusu kutengeneza barabara ya Kitulo kwenda Busokelo; hii barabara haikuwepo, ni mpya. Atakubaliana nami kwamba tumeshaanza kuifungua na tumeifungua yote, kinachosubiriwa sasa ni kuikamilisha, kwa maana ya kujenga makalavati na kuweka changarawe ili kuhakikisha kwamba wananchi wa pande hizi mbili wanaweza kuwasiliana, na hasa wananchi wa Busokelo kwenda Hospitali ya Ikonda ambao wanaihitaji sana, ahsante.

Name

Esther Edwin Maleko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FESTO R. SANGA aliuliza: - Je, ni hatua gani ya upembuzi yakinifu wa barabara ya Chimala – Matamba hadi Kitulo imefikiwa na lini ujenzi utaanza?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER E. MALLEKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru: -

Je, ni lini Serikali itafanya upembuzi yakinifu kwa barabara ya Mwembe-Mbaga na hatimaye kuijenga kwa kiwango cha lami kwa sababu imekuwa ni changamoto kubwa sana kwa wakazi wa milimani?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Mbunge awe na Subira, barabara nyingi sana tunategemea kuzifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Tukiwa tunajua tunaelekea mwisho wa utekelezaji wa ilani ya chama, kwa hiyo tunaamini barabara zote ambazo zimeainishwa kufanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina tutazifanya kuanzia mwaka huu na mwaka ujao wa fedha, ikiwepo na barabara ya Mheshimiwa Mbunge aliyoisema, ahsante.

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. FESTO R. SANGA aliuliza: - Je, ni hatua gani ya upembuzi yakinifu wa barabara ya Chimala – Matamba hadi Kitulo imefikiwa na lini ujenzi utaanza?

Supplementary Question 3

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante; Barabara ya Mpunze-sabasabini ipo Nyagholo mpaka Igwamanoni imekatikakatika haipitiki kabisa na imepandishwa kutoka TARURA kwenda TANROADS. Ni nini mkakati wa Serikali kwa ajili ya kuijenga barabara hii angalau hata kujua maeneo yaliyokatika ili wananchi waweze kupita kwa urahisi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cherehani, Mbunge wa Ushetu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli barabara aliyoitaja ilikuwa inahudumiwa na wenzetu wa TARURA, na ndiyo kwanza imekuja sasa TANROADS. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa wa Ushetu pamoja na wananchi wa Ushetu, kwamba tumesikia, na ninamwagiza Meneja wa Mkoa wa Shinyanga, cha kwanza aende akahakikishe kwamba yale maeneo yote ambayo yamekatika anayarejesha ili kuwe na mawasiliano. Pia aweze kufanya tathmini ili maeneo yote yale korofi tuweze kuangalia namna ya kuyarakabati vizuri ili yaweze kupitika muda wote hata kipindi cha masika, ahsante.

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. FESTO R. SANGA aliuliza: - Je, ni hatua gani ya upembuzi yakinifu wa barabara ya Chimala – Matamba hadi Kitulo imefikiwa na lini ujenzi utaanza?

Supplementary Question 4

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi. Barabara ya Mafinga Mgololo inapita katika majimbo matatu, kwa maana ya Mafinga Mjini, Mufindi Kaskazini na Mufindi Kusini. Katika majibu ya Serikali mara zote wanasema kwamba barabara hii iko chini ya utaratibu wa EPC+F, na kwamba Wizara ya Ujenzi wao wameshamaliza kazi suala hili liko hazina. Sasa wananchi wa Wilaya ya Mufindi wanatuuliza sisi Wabunge wao watatu, kwamba;

Je, hawa wa ujenzi hawawezi kwenda huko fedha kuwaambia sasa watoe fedha hii barabara ianzwe kujengwa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Chumi, Mbunge wa Mafinga Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimwakikishie Mheshimiwa Chumi, Mheshimiwa Kihenzile na Mheshimiwa Kigahe, kwamba barabara aliyoitaja ya hawa Wabunge wote ipo na hakuna barabara ambayo imeachwa katika huu mpango wa EPC+F. Kwa kweli taratibu zinakwenda vizuri tupo tunakamilisha taratibu na nadhani kipindi cha bajeti hizi barabara zote nategemea tutaziwakilisha na zianze utekelezaji, ikiwepo na barabara ya Mgololo hadi Mafinga, ahsante.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. FESTO R. SANGA aliuliza: - Je, ni hatua gani ya upembuzi yakinifu wa barabara ya Chimala – Matamba hadi Kitulo imefikiwa na lini ujenzi utaanza?

Supplementary Question 5

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Sera ya Taifa letu ni kuunganisha barabara za mikoa kwa lami, lakini sisi Mkoa wa Lindi haujaunganishwa na Mkoa wa Morogoro kwa barabara hata ya vumbi.

Je, Serikali inasema nini juu ya kuunganisha sisi Mkoa wa Morogoro na Lindi kwa barabara angalau ya changarawe pale Liwale na Mahenge?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka Mbunge wa Liwale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimwakikishie Mheshimiwa Mbunge Kuchauka, kwamba mwaka huu wa bajeti tumependekeza kwanza tufanye upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kati ya Liwale, Ilonga hadi Mahenge ili hii barabara tuweze kuifungua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii barabara inapita kwenye Mbuga ya Selous, na limekuwa ni ombi kubwa sana la wanalindi akiwepo Mheshimiwa Kuchauka sasa tumeiweka kwenye mpango wa kuifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Kwa hiyo kama bajeti yetu itapita tuna uhakika hiyo kazi itakuwa imeanza kuunganisha Mkoa wa Lindi na Mkoa wa Morogoro, ahsante.

Name

Furaha Ntengo Matondo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FESTO R. SANGA aliuliza: - Je, ni hatua gani ya upembuzi yakinifu wa barabara ya Chimala – Matamba hadi Kitulo imefikiwa na lini ujenzi utaanza?

Supplementary Question 6

MHE. FURAHA N. MATONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami Barabara ya Mwanango kupita Kahama inayounganisha Mkoa wa Shinyanga ili kukuza uchumi na ipo kwenye ilani ya uchaguzi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Furaha Matondo, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mwanza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii tulishakamilisha usanifu wa kina na tumeanza kuijenga kwa hatua na hasa maeneo ambayo ni ya mijini, ikiwa ni mpango wa Serikali kutafuta fedha kuijenga barabara ya Mwanangwa-Solwa hadi Kahama kwa kiwango cha lami, ahsante.