Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 13 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 168 2023-04-25

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. FESTO R. SANGA aliuliza: -

Je, ni hatua gani ya upembuzi yakinifu wa barabara ya Chimala – Matamba hadi Kitulo imefikiwa na lini ujenzi utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Festo Richard Sanga, Mbunge wa Makete kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Chimala – Matamba yenye urefu wa kilometa 20.1 ni barabara ya Wilaya ambayo imekasimiwa kwa TANROADS kuanzia mwaka wa fedha 2023/2024. Baada ya kukasimiwa TANROADS, barabara yote kuanzia Chimala – Matamba hadi Kitulo ambayo itakuwa na urefu wa kilometa 41.1 itaingizwa kwenye mpango wa kufanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami katika mwaka wa fedha wa 2023/2024, ahsante.