Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza: - Je, lini vituo vidogo vya treni vya Njage na Itongowa katika reli ya TAZARA vitarejeshwa?

Supplementary Question 1

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza kama ifuatavyo (a) na (b): -

(a) Ningependa kujua kwa kupata commitment ya Serikali, ni lini sasa vituo hivi vitarejeshwa?

(b) Wananchi wa maeneo haya Njage na Itongowa wamekuwa wakipata adha kubwa sana ya usafiri hasa ukizingatia wakati huu wa masika sisi Wananchi wa Mlimba usafiri wetu mkubwa ni treni ya TAZARA. Sasa namwomba Mheshimiwa Naibu Waziri lini atakuwa tayari kuambatana nami tupande treni hiyo ya TAZARA anaposema hapo Ifakara mpaka Mbingu tushuke kwenda Njabi umbali wa kilometa tisa halafu apate hiyo adha na yeye ataona najua atachukua hatua. (Makofi)

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Godwin Emmanuel Kunambi Mbunge wa Mlimba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimwakikishie Mheshimiwa Mbunge pamoja na wananchi wote wanaotumia vituo hivi vya Stesheni ya Reli ya TAZARA kwamba tarehe 28 Ijumaa ya wiki hii tunatuma timu ya wataalam kwenda kufanya tathmini ya kina. Itafanya kazi hii kwa wiki moja, mpaka tarehe 06 ya mwezi wa tano, na watatoa taarifa ama ripoti ambayo hiyo itakuwa msingi wake katika kufanya maamuzi. Hata hivyo swali lake la pili ni lini kwenda huko, Mheshimiwa Mbunge mimi na wewe nitakwenda pamoja na wewe siku ya weekend wakati vikao vya Bunge vinaendelea, tutaomba ruhusa kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu na Spika ili twende kuona adha hii kwa wananchi na hatimaye kufanya maamuzi sahihi.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza: - Je, lini vituo vidogo vya treni vya Njage na Itongowa katika reli ya TAZARA vitarejeshwa?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, swali langu ni dogo; kwa kuwa huduma ya treni ya mwendokasi nchini inasubiriwa kwa hamu kubwa sana.

Je, ni lini shirika hili litaanza kutoa huduma kati ya Dar es Salaam na Dodoma?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zacharia Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Reli yetu ya TRC hususan katika mradi wetu wa SGR kutoka Dar es Salaam – Morogoro – Dodoma awamu ya kwanza tutaanza kutoa huduma kuanzia Dar es Salaam hadi Morogoro. Hivi ninavyosema tumeshafanya testing katika vituo vyote signal na treni la Mkandarasi na kwa maana hiyo tunachosubiria sasa ni kuja vichwa na hivi vichwa tunategemea vitakuja ndani ya mwezi ujao ili ianze kufanya hii station ya SGR, ahsante.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza: - Je, lini vituo vidogo vya treni vya Njage na Itongowa katika reli ya TAZARA vitarejeshwa?

Supplementary Question 3

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwanza naomba nitoe pole nyingi kwa wananchi wa Jimbo la Hai kutokana na mafuriko yanayoendelea sasa hivi kwenye maeneo mbalimbali. Swali langu, ni lini Serikali itajenga kituo kidogo cha treni eneo la Rundugai sokoni?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Saashisha Mbunge wa Hai kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, natambau kwamba kituo hiki cha reli, treni ya abiria inayotoka Dar es Salaam kwenda Arusha ni miongoni mwa maeneo ambayo pia tunashusha. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tunaweka fedha kwenye bajeti ijayo, nitaomba wakati wa kupitisha Bajeti ya Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi tuunge mkono ili tujenge kituo hiki kiweze kutumika, ahsante.