Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 13 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 167 2023-04-25

Name

Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza: -

Je, lini vituo vidogo vya treni vya Njage na Itongowa katika reli ya TAZARA vitarejeshwa?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Godwin Emmanuel Kunambi, Mbunge wa Mlimba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, TAZARA ilipokea barua za maombi ya kufunguliwa kwa vituo vidogo vya Njage na Itongowa katika vipindi tofauti tangu mwaka 2022. Tathmini iliyofanywa ilibainisha yafuatayo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kituo kidogo cha Itongowa. Kituo hiki kinachoombwa kuanzishwa kipo kati ya Stesheni kubwa za Chita na Mngeta. Katikati ya Stesheni mbili hizo za Chita na Mngeta kipo kituo kidogo cha siku nyingi cha Ikule. Kituo hiki cha Ikule kipo kilometa sita kutoka aidha Chita ama Mngeta. Kituo cha Itongowa kinachoombwa kuanzishwa kitakuwa kilometa sita kutoka Mngeta stesheni au kilometa saba kutoka Ikule.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kituo kidogo cha Njage. Kituo hiki kinachoombwa cha Njage kipo kati ya Stesheni kubwa za Mngeta na Mbingu ambazo treni za abiria zinasimama. Umbali kati ya stesheni hizo ni kilometa 18 yaani Mngeta na Mbingu. Kitongoji cha Njage kipo katikati Mngeta na Mbingu yaani kilometa tisa kutoka kila upande, Mngeta au Mbingu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo Wizara imeelekeza sasa TAZARA ifanye tathmini ya haraka kwa kina kuona uwezekano wa kuanzisha vituo hivi vilivyoombwa na Mheshimiwa Mbunge ili wananchi wasitembee umbali mrefu.