Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa mradi wa maji wa Kyerwa, Nyaruzumbura, Nyakatuntu hadi Kamuli Wilayani Kyerwa?

Supplementary Question 1

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Mradi wa Kilela, Lutunguru na Isingiro, mradi huu unajengwa kwa awamu mbili, mkandarasi anakaribia kukamilisha awamu ya kwanza. Ni lini Serikali itatangaza awamu ya pili ili mradi huu uweze kukamililka? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Wataalamu walifika kwenye Kata ya Businde, Bugala, Kibale pamoja na Kikukuru wakapima vijiji vichache ili wananchi waweze kupatiwa maji lakini adha ni kubwa wananchi wanayoipata. Je, Serikali iko tayari kupima vijiji vyote vya kata hizo ili wananchi hawa waweze kupatiwa maji safi na salama? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Innocent Bilakwate kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli mradi ule wa kwanza alioutaja unaopita kwenye vijiji vya Kilela, Lutunguru ni kweli awamu ya kwanza umeshakamilika na sasa tunaelekea kwenye usambazaji na tunatarajia mwezi Mei kuweza kuutangaza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la pili, maeneo ambayo ameyataja Mheshimiwa Mbunge ni kweli vijiji vilishapimwa na tayari tunaendelea na utaratibu wa kuona kwamba maeneo haya yote ambayo miundombinu ya maji kuyapitia iko mbali basi tuweze kuchimba visima na tayari tumshukuru Mheshimiwa Rais ile mashine ambayo ilipaswa kufika Mkoa wa Kagera sasa inatarajiwa kutoka Karagwe na kuelekea Kyerwa lakini vile vile vijiji ambavyo havikupimwa tunavitarajia navyo vipimwe viingie kwenye mpango wa kupata maji safi na salama.

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa mradi wa maji wa Kyerwa, Nyaruzumbura, Nyakatuntu hadi Kamuli Wilayani Kyerwa?

Supplementary Question 2

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Jimbo langu la Kalenga limekuwa halina chanzo cha uhakika cha maji ambacho kinaweza kikapeleka maji kwenye kata zaidi ya moja. Mfano Kata ya Masaka haina maji kabisa. Je, ni lini sasa Serikali itatafuta chanzo kimoja kikubwa ili tuweze kupeleka maji zaidi ya kata moja? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kiswaga, Mbunge wa Kalenga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli maeneo haya anayotaja Mheshimiwa Mbunge ambaye ni Mwenyekiti wetu wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira. Ni kweli vyanzo vyake vinapata changamoto kama chanzo kile cha Nyamlenge kwa sasa tunashuhudia wote kwamba kinaendelea kujaa mchanga lakini watu wetu wa bonde wanaendelea kufanya kazi nzuri kuhakikisha vyanzo vinabaki salama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa maeneo yote ya Kalenga tunaendelea kufanya utafiti, tunatarajia kutumia labda Mto Lyandemberwa ambao unaweza ukasaidia eneo la Kalenga kupata maji safi na salama yakiwa bombani.

Name

Eng. Dr. Leonard Madaraka Chamuriho

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa mradi wa maji wa Kyerwa, Nyaruzumbura, Nyakatuntu hadi Kamuli Wilayani Kyerwa?

Supplementary Question 3

MHE. ENG. DKT. LEONARD M. CHAMURIHO: Mheshimiwa
Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia fursa hii ya kuuliza swali. Kijiji cha Kyabakari kimekosa huduma ya maji kwa muda wa miezi mitatu sasa. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba kijiji hicho kinapata maji japo kuwa kuna mradi mkubwa wa maji? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Leonard Chamuriho kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kijiji ambacho kinaweza kikakosa maji miezi mitatu na tayari kina miundombinu ya maji ni suala la kufuatilia changamoto ilipo. Naomba nilichukue tutahakikisha maji yanarejea kwa wananchi ili kuondokana na kero ambayo wanaipata kwa sasa.