Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: - Je, lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya kukamilisha Mradi wa Skimu ya Umwagiliaji wa Kyakakera uliopo katika Kata ya Kyaka?

Supplementary Question 1

MHE. FLORENT L. KYOMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nishukuru kwa majibu ya Serikali japo niseme nina imani sana na Mheshimiwa Bashe na Mheshimiwa Antony Mavunde kwa sababu skimu hii imekuwa ni muda mrefu imetelekezwa bila mafanikio. Naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, skimu hii imeshatumia zaidi ya shilingi milioni 944 ambazo hazikuleta tija yoyote. Je, ni nini commitment ya Serikali kuhakikisha kwamba sasa inaumalizia mradi huo na unakuwa na tija kwa wananchi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Wakulima wa eneo hilo walisimamishwa kuendelea na ulimaji katika skimu hiyo mwaka 2013, leo ni miaka 10 tunapoongea hakuna chochote kinachoendelea. Naomba Serikali itoe matumaini kwa wananchi hao kuweka commitment kwamba sasa skimu hii inaenda kukamilishwa na wananchi wanarudi pale kwa ajili ya kulima kilimo cha umwagiliaji na kuleta tija katika maisha yao?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza ni commitment. Nataka nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge, ni dhamira ya Serikali ya kuhakikisha ya kwamba tunaendeleza kilimo cha umwagiliaji kupitia miradi mbalimbali. Mradi wa Kyakakera ambao umekaa muda mrefu ni mkombozi mkubwa wa wakulima. Tumekwisha mwelekeza Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kuhakikisha wanalipitia eneo hili na tulikamilishe kwa haraka ili wakulima wetu waanze kutumia mradi huu kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, sisi wenyewe hatupendi kumwona Mkulima amekaa bila kufanya kilimo lakini mradi huo ulikuwa chini ya DADP na ziko changamoto ambazo zilijitokeza katika utekelezaji wa hii miradi na hivi sasa tumejikita kuhakikisha kwamba tumejenga miradi ambayo itakuwa ni bora na ya kudumu muda mrefu ili wakulima wetu wasipate shida. Miaka 10 ya wakulima ni mingi nataka nikafute kilio hicho kwamba Mkurugenzi Mkuu akienda huko aifanye kazi hiyo vyema wakulima hao waweze kuanza kulima mapema kabisa katika msimu unaokuja hivi karibuni.

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: - Je, lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya kukamilisha Mradi wa Skimu ya Umwagiliaji wa Kyakakera uliopo katika Kata ya Kyaka?

Supplementary Question 2

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuweza kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichukue nafasi hii kuishukuru Serikali kwa kutenga zaidi shilingi milioni 900 kwa ajili ya ujenzi wa Skimu ya Umwagiliaji ya Endagaw. Kwa sasa mkandarasi ameweza kusimamishwa. Je, ni lini Serikali itatuletea mkandarasi ili aweze kukamilisha ujenzi wa skimu hiyo na uweze kuleta tija kwa fedha za Serikali lakini kwa wananchi pia? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru Mbunge amekuwa mfuatiliaji mzuri katika eneo hili. Ni kweli mkandarasi aliyekuwepo Endagaw tulimsimamisha na kumwondoa lakini tuko katika hatua za mwisho za kumpata mkandarasi mwingine ambaye atakwenda kukamilisha kazi hiyo kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge wape tu matumaini wakulima wako kwamba kazi itakamilika na watafanya kilimo cha umwagiliaji.

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: - Je, lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya kukamilisha Mradi wa Skimu ya Umwagiliaji wa Kyakakera uliopo katika Kata ya Kyaka?

Supplementary Question 3

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Kwa bajeti inayoendelea sasa Bunge hili lilipitisha uanzishwaji wa Skimu ya Ibanda Geita na Igaka Sengerema. Ni lini utekelezaji wa skimu hii utaanza?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi wa Ibanda ni moja kati ya miradi muhimu sana katika Mkoa wa Geita na hususan Jimboni kwa Mheshimiwa Kanyasu. Habari njema ni kwamba tumekwisha kutangaza juu ya Bwawa la Ibanda na muda siyo mrefu pia tutatangaza kumpata mkandarasi kwa ajili ya skimu.