Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 13 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 164 2023-04-25

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: -

Je, lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya kukamilisha Mradi wa Skimu ya Umwagiliaji wa Kyakakera uliopo katika Kata ya Kyaka?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Florent Laurent Kyombo Mbunge wa Nkenge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Skimu ya umwagiliaji ya Kyakakera ni miongoni mwa skimu zinazounda Bonde la Mto Ngono lenye ukubwa wa hekta 11,700 zinazofaa kwa kilimo cha umwagiliaji ambapo kupitia bajeti ya mwaka 2022/2023 Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imetenga fedha kwa ajili ya kufanya mapitio ya upembuzi yakinifu na kufanya usanifu wa kina. Mpaka sasa, Serikali ipo katika hatua za kukamilisha manunuzi ya kumpata mshauri mwelekezi atakayefanya kazi hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, katika Mpango na Bajeti ya Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kwa mwaka wa fedha 2023/2024 Bonde la Mto Ngono limetengewa bajeti ya ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji ambapo jumla ya hekta 3,000 zimepangwa kuendelezwa katika mwaka wa kwanza wa utekelezaji na Skimu ya Kyakakera itakuwa miongoni mwa skimu za awamu ya kwanza zitakazoendelezwa wakati wa utekelezaji wa ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji katika Skimu ya Bonde la Mto Ngono.