Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga nyumba za madaktari wa Hospitali ya Mkoa wa Iringa?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri. Vile vile nitoe masikitiko yangu makubwa sana kwa haya majibu aliyotoa, kwa sababu mchakato huu wa kuhamisha gereza ili hospitali iweze kufanya kazi vizuri siyo wa leo wala wa jana, ni wa muda mrefu sana; je, huu mchakato ni lini utakamilika? Kwa sababu haya majibu nimekuwa nikipatiwa muda mrefu, naomba leo anipe jibu, lakini siyo la mchakato tena. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili. Kwa niaba ya akina mama wa Mkoa wa Iringa naomba kumpongeza Daktari Bingwa wa Magonjwa ya akina mama, Dkt. Mwakalebela. Kwa kweli anawatendea haki akina mama, na vifo vya watoto vimepungua; lakini tunayo changamoto ya muda mrefu sana kwa Daktari Bigwa wa Upasuaji wa Mifupa. Wananchi wa Iringa wanapata ajali nyingi sana, hata jana kuna ajali pale Kitonga imetokea; hili tatizo tumeshalileta muda mrefu Serikali, lakini hatupatiwi Daktari, wananchi wanapata shida kuja Dodoma au kwenda Dar es Salaam: Je, ni lini sasa huyu Daktari Bingwa wa Upasuaji atakuja katika Mkoa wetu wa Iringa? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwanza kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa jinsi anavyofuatilia huduma za afya, siyo tu kwa Hospitali ya Mkoa wa Iringa, lakini kwa Wilaya zake za Mkoa wa Iringa kwa kushirikiana na Waheshimiwa Wabunge wa Majimbo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la kwanza ni mchakato utaisha lini? Namwomba Mheshimiwa Mbunge, mimi na yeye twende pamoja Wizarani na tutamwonyesha mchakato ulipofikia na tutaendelea kwa pamoja tuumalize.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukizungumzia Hospitali ya Mkoa, siyo suala la majengo tu, ni suala la skills zilizopo pale na teknolojia iliyosimikwa kwenye hospitali. Kwa hiyo, ni kazi. Ukisema uchomoe hiyo teknolojia haraka ukahamisha, utavuruga huduma za afya kwenye mkoa. Kwa hiyo, ndiyo maana mambo mengi yanachelewa pamoja na mawasiliano na Wizara ya Mambo ya Ndani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili kuhusu Daktari Bingwa wa Mifupa, kama alivyosema Mheshimiwa Waziri wa Afya, Bunge liliopita, kwa hospitali yetu ya Iringa kwa mchakato unaoendelea sasa hivi ndani ya Wizara kuhamisha madaktari, Iringa wanahitaji kupelekewa Daktari wa Mifupa, Daktari wa ENT na Daktari wa Neurologist. Kwa hiyo, tumelipokea na litafanyiwa kazi mara moja. (Makofi)

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga nyumba za madaktari wa Hospitali ya Mkoa wa Iringa?

Supplementary Question 2

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Hospitali ya Manyamanyama inatoa huduma kwa wananchi wa zaidi ya Mkoa wa Mara pale Bunda Mjini, lakini wana changamoto ya nyumba ya watumishi wa afya. Ni lini sasa mtatupatia nyumba mbili ya watumishi wa afya katika Hospitali ya Manyamanyama? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimwambie Mbunge hongera kwa swali lake zuri, nawakumbuka watu wake huko Bunda. Nimwambie tu kwamba kwa nafasi zilizotolewa zaidi ya 21,000 tutashirikiana na wenzetu wa TAMISEMI tuone ni namna gani tunaweza tukatatua hilo tatizo mapema zaidi kwenye nafasi zilizotoka sasa.