Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 13 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 162 2023-04-25

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga nyumba za madaktari wa Hospitali ya Mkoa wa Iringa?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Ritta Enespher Kabati, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali imejenga nyumba 50 za watumishi zenye thamani ya shilingi bilioni 3.4 katika Hospitali za Kanda na Hospitali za Rufaa za Mikoa ikiwemo nyumba moja katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mashauriano yanaendelea ndani ya Serikali ili kukamilisha mchakato wa kuhamisha gereza la mkoa ili kutoa nafasi ambayo itawezesha Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa kuendelea na upanuzi wa huduma mbalimbali ikiwemo ni pamoja na ujenzi wa nyumba za Madaktari.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.