Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, lini Wananchi wa Busanda watapatiwa Wilaya ya Busanda kama ilivyopendekezwa na Baraza la Madiwani, DCC na RCC Geita?

Supplementary Question 1

MHE. TUMAINI B. MAGESSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa kuwa uboreshaji huu ni kazi ambayo imepangwa (planned activity): Je, Serikali imepanga kukamilisha lini hii kazi ya uboreshaji wa maeneo ambayo iliyaanzisha?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili: Jimbo la Busanda lina wananchi takribani zaidi ya 700,000; ina kata 22, lakini ina tarafa mbili tu: Ni lini Serikali itaongeza idadi ya tarafa ili wananchi waweze kufikiwa kwa urahisi zaidi? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa
Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Tumaini Bryceson Magessa, Mbunge wa Jimbo la Busanda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, uboreshaji wa miundombinu katika Halmashauri zetu ni zoezi ambalo sasa linaendelea na Serikali imeshajenga majengo mapya ya Halmashauri zaidi ya 115 na inaendelea na ujenzi wa majengo ya Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, na pia tutakwenda kwenye ngazi za kata. Kwa hiyo, zoezi hili ambalo linaendelea kutekelezwa ni la muda, na mara litakapokamilika kutokana na upatikanaji wa fedha, basi tutakwenda kwenye hatua nyingine ya kuona uwezekano wa kuanzisha mamlaka nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, kuhusiana na kuanzisha tarafa katika Jimbo hili la Busanda, namwomba Mheshimiwa Mbunge na pia nielekeze Halmashauri kufuata taratibu za uanzishwaji wa tarafa, kwa maana ya kufanya vikao kwenye ngazi ya DCC, RCC na kuwasilisha kwenye Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili tathmini ifanyike na hatua stahiki ziweze kuchukuliwa, ahsante.

Name

Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, lini Wananchi wa Busanda watapatiwa Wilaya ya Busanda kama ilivyopendekezwa na Baraza la Madiwani, DCC na RCC Geita?

Supplementary Question 2

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Vikao vya DCC na RCC wakati mwingine majibu yake yanachelewa kutoka Serikalini: Je, ni lini Serikali itatupatia majibu ya mabadiliko ya jina la Mji wa Mugumu kuwa Mji wa Serengeti kama lilivyopitishwa na vikao vya DCC na RCC? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Amsabi Mrimi, Mbunge wa Jimbo la Serengeti, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imetoa maelekezo na utaratibu wa taarifa na maamuzi na mapendekezo ya DCC na RCC kuletwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI yako wazi. Nisisitize kwamba baada ya vikao hivyo, Makatibu Tawala wa Mikoa wahakikishe kwamba taarifa zinafika Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu jina la Mugumu kwenda kuwa Serengeti, naomba tulichukue hili tukatazame limefikia hatua gani, tuone maoni ya wadau na baadaye Serikali itatoa maamuzi lipi linakwenda kufanyika? Ahsante sana.