Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 13 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 161 2023-04-25

Name

Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: -

Je, lini Wananchi wa Busanda watapatiwa Wilaya ya Busanda kama ilivyopendekezwa na Baraza la Madiwani, DCC na RCC Geita?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tumaini Bryceson Magessa, Mbunge wa Jimbo la Busanda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mnamo tarehe 24/02/2021 Mkoa wa Geita uliwasilisha mapendekezo ya kuanzisha Wilaya mpya ya Busanda kwa kugawa maeneo ya Wilaya za Geita na Chato. Kwa kuwa mamlaka nyingi zilizoanzishwa bado zina upungufu wa miundombinu mbalimbali yakiwemo majengo ya utawala na huduma za kijamii, kwa sasa Serikali imeweka kipaumbele katika kuboresha miundombinu katika maeneo ya utawala yaliyopo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itakapokamilisha maboresho ya miundombinu na huduma kwenye mamlaka zilizoanzishwa, itaendelea na taratibu za uanzishwaji wa maeneo mapya ya utawala ambayo yatakakidhi vigezo, ahsante.